Thursday 25 September 2014

HOTEL YA BLUE PEAR YA UBUNGO YAFUNGWA KISA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Filled under:

 
Fanicha za hoteli ya Blue Pearl viitolewa nje. (picha: The Citizen)
Huduma za hoteli ya Blue Pear ya Ubungo jijini Dar es Salaam imefungwa baada ya mmiliki kuripotiwa kushindwa kulipa fedha ya pango inayokadiriwa kufikia shilingi bilioni sita ($3,800,000).
Gazeti la The CITIZEN linaripoti kuwa juzi mchana maafisa wa kampuni ya Majembe Auction Mart walifika katika eneo la hoteli hiyo na kuanza kutoa fanicha nje kisha kuzipakia kwenye lori.
Wateja waliambiwa wahame kutoka kwenye eneo la hoteli hiyo kwa kuwa ilikuwa imefungwa na huduma kusitishwa.
Mr Seth Motto wa Majembe Auction Mart alisema kampuni yake ilipewa jukumu hilo na menejimenti ya Ubungo Plaza Ltd, ambao ni wamiliki wa jengo hilo.

Posted By Unknown23:50

VIPEPERUSHI VYENYE MANENO YA VITISHO VYASAMBAZWA DODOMA

Filled under:


WanaCCm walifika katika jengo lao leo Alhamisi, Septemba 25, 2014, Dodoma na kukuta limeandikwa maneno kwa rangi nyekundu "NO KATIBA UFISADI " na kama hilo halitoshi kukawepo vipepersuhi vinasambazwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME - SACP amesema tarehe 25/09/2014 alfajiri vimeokotwa vipeperushi maeneo mbalimbali mjini Dodoma vyenye ujumbe ufuatao: ONYO – DODOMA SI MAHALI PA KUFUGA WEZI WA FEDHA ZA UMMA. UTAKAYEINGIA BUNGENI KUANZIA KESHO, YATAKAYOKUPATA UTAJUTA.
Kamanda MISIME amesema tumeendelea kupokea taarifa za watu wanaodaiwa kuandaa vipeperushi hivyo na tunafanyia kazi ili tuweze kuwakamata ili washtakiwe kulingana na kosa walilolitenda hasa la kutoa vitisho na kuhamasisha uvunjifu wa amani.

Aidha Kamanda MISIME ameongeza ametoa wito kwa wananchi na wageni wanaofika Dodoma watii sheria bila shuruti. Kila mmoja ajiepushe kujiingiza kwenye kuhamasisha uvunjifu wa amani, kujiingiza katika mikusanyiko isiyo halali na maandamano ambayo yameshapigwa marufuku na Jeshi la Polisi.

Atakayekiuka na kujiingiza katika vitendo hivyo vya kiuhalifu atashurutishwa kwa nguvu zote kwa mujibu wa sheria za Nchi na kwa mamlaka iliyopewa Jeshi la Polisi.

Kamanda MISIME ameongeza kuwa wananchi na wageni wapenda amani waendelee na shughuli zao kama kawaida kwani Jeshi la Polisi limejiimarisha ipasavyo kukabiliana na yeyote yule atakayekiuka sheria na maelekezo yaliyotolewa.


  • Taarifa ya Sylvester Onesmo wa Jeshi la Polisi, Dodoma.

Posted By Unknown23:27

WARAKA WA MLIMANDAGO ALIVYOMCHAFUA DIALO KWA KUMLIPUA LOWASA

Filled under:

NAIBU Waziri wa zamani wa Maji, Anthony Diallo, amesema dhana inayojengwa kwamba Mradi wa Maji wa Ziwa Victoria ulifanikishwa kwa nguvu ya aliyekuwa Waziri, Edward Lowassa, ni potofu na afadhali angetajwa yeye.

Katika mazungumzo na Raia Mwema yaliyofanyika mjini Mwanza wiki hii na ambayo yatachapishwa katika gazeti dada la hili la Raia Tanzania kesho, Diallo ambaye sasa ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mwanza, ameweka wazi kwa kila hatua kuhusu mradi huo.

Kimsingi, Diallo ameeleza kwamba mradi huo wa maji ulitokana na ahadi iliyotolewa na Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, kwa wananchi wa Kanda ya Ziwa mwaka 2000 na kama ingekuwa sifa ni bora zingeenda kwake.

“Kwanza kuna vitu viwili. Cha kwanza miradi yote inayolipiwa na kodi za wananchi ni jukumu la serikali iliyoko madarakani, sidhani anaweza kutokea mtu mmoja kudai kwamba nilifanikisha hiki.
Ukienda kwa staili hiyo ndiyo watu wanasema ile dhana ya wabunge kuwa mawaziri inaleta haya matatizo kwamba mtu anavutia kwake akiwa na nia fulani, sasa hao wanaodai kwamba walifanya hivi definitely lazima ujue kwamba wana nia fulani, wanataka kuwavutia wapiga kura kwamba wao wanawajali sana.

Sitakueleza mambo ambayo ni siri ya Baraza la Mawaziri, siwezi kuitoa, lakini moja ni kwamba mradi huo ulikuwa ahadi ya Rais Mkapa, mwaka 2000 wakati anaomba kura kipindi cha pili, alipopita Shinyanga na Kahama alisema lazima tufanye chini juu tutajenga mradi wa maji kuelekea huko kutoka Ziwa Victoria.

Sasa ngoma ilikuwa ni pesa zitapatikana wapi, mwaka 2002 tukaanza mazungumzo makali sana na nchi hizi zilizo kwenye Bonde la Nile, na bahati nzuri mimi ndiye nilihudhuria vikao vyote, mpaka tukafika mahali tukauvunja ule mkataba wa Misri na Uingereza, kwa sababu walikuwa wanatuzuia tusitumie maji ya Ziwa Victoria na hiyo mikutano yote nimehudhuria mimi, Addis Ababa. Na nimshukuru sana waziri mwingine aliyenisaidia, maana nilikuwa vocal sana, Martha Karua wa Kenya, aliyekuwa Waziri wa Maji wakati huo,”

alisema Diallo.

Kauli hii ya Diallo ni ya kwanza kutamkwa hadharani kuhusiana na mradi huo ambao mara nyingi
umekuwa ukitajwa na wapambe wa Lowassa kuwa kati ya kete zake muhimu ndani ya chama chake kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwakani.

Wapambe hao wamekuwa wakisema ni Lowassa aliyeusukuma na kuusimamia tangia kwenye mchakato wa kuondoa tatizo la maji kwa wananchi wa Kanda ya Ziwa, hasa Shinyanga na Kahama.

Katika mazungumzo hayo, Diallo alieleza ya kuwa akiwa Naibu Waziri chini ya Lowassa, namna alivyoshiriki katika kila hatua kabla ya kuhamishwa wizara.

“Baada ya hapo ikaja ngoma kwamba huu mradi utapate pesa kutoka wapi. Mimi nikafanya utafiti mdogo nikagundua kwamba tusingeweza kupata hela za wahisani kokote kwa sababu World Bank (Benki ya Dunia) jamaa wa Misri wamejaa hata IMF (Shirika la Fedha Duniani) kote kule wamejaa.

Lakini pia tukakumbuka miaka ya 1960 tulipokazana kuchukua haya maji kwenye mradi ule wa Wendele, nchi za Scandinavia zikazuia kwamba tusichukue maji Ziwa Victoria badala yake wakasema tuchimbe malambo, yakaja matrekta mengi na kwa sababu tulikuwa hatuna ufundi matrekta hayo mengi yamekuja kukusanywa kwenye vyuma chakavu, kama unakumbuka kulikuwa na katapila karibu kila kijiji mengi yamekuja kukusanywa kama vyuma chakavu. Kwa hiyo ilikuwa ni tabu sana pesa mtapata wapi.

Nikaja na wazo kwamba kwanini tusiombe pesa kwa Rais, tutumie pesa zetu wenyewe, wakati huo pesa za makusanyo ya kodi zilianza kupanda sana. Basi tukamwandikia barua Rais, tukamwambia uwezekano wa kupata funding ni mdogo sana, kwa hiyo akakubali tutumie pesa zetu wenyewe.

Wakati ule huo mradi ulikadiriwa kumalizika kwa bilioni 27. Mimi nikaja na wazo pale wizarani, nikawaambia kwa pesa hiyo huu mradi hauwezi kuisha , kwanini tusilishawishi Baraza la Mawaziri tufanye kwa awamu, tukaandika mradi wetu na matarajio yote tukakubaliwa.

Ili tujenge kwanza pampu na lile tenki la Ihelele (kijiji kando ya ziwa unakoanzia mradi huo) hiyo ilikuwa awamu ya kwanza bilioni 27 zingeishia hapo. Nikawa nawatania wizarani kwamba tukishafikisha maji pale (Ihelele) hakuna Wizara itakayopinga tusichukue hela kuyapeleka maji mbele.

Awamu ya pili ilikuwa umeme tutaupata wapi, kwa sababu pale (kwenye chanzo cha maji) ni porini tu, mara ya kwanza tukakubaliana kwamba tujenge sub station (kituo kidogo) lakini Tanesco hawakuwa waangalifu sana ule mradi tukaliwa, kwa sababu waliweka nguzo na nyaya ambazo ni sub standard (chini ya kiwango) zisingeweza kuendesha yale mapampu.

Tukaja na wazo la kuchukua umeme Kahama Mining, ikadibi tufanye hivyo, zile nguzo za awali zikatelekezwa. Hapo serikali tulikula hasara, ingawa si mbaya kwa sababu tulikuwa tunafanya kitu kinaitwa learning curve na watalamu wetu hawakuwa wazuri kiasi hicho.

Idea ya pili niliyoitoa mimi, nilikuwa mtu wa kwanza kuleta ule utaratibu wa design and build, nikawaambia hapa tukitaka tuweke feasibility study (upembuzi yakinifu), tutazeekea hapo mradi hautakamilika.

Kwa hiyo mkandarasi tutakayempa atakuwa ana design, tunaipitia design (michoro) yake na consultant (mtaalam mshauri) tutakuwa tumeshamuweka tunakubaliana anajenga ili mradi tunajua bei haiwezi kuvuka hapo.

Hata mkimuuliza Waziri Lowassa (Edward Lowassa Waziri wa Maji wakati huo) anakumbuka. Ule mradi ulikuwa mikononi mwangu, yeye alikuwa anashughulikia DAWASA. Tulikubaliana kugawana mimi nisimamie mradi wa Shinyanga yeye asimamie DAWASA, nilikuwa na maamuzi yote.

Huo mradi ndiyo ulikuwa hivyo, lakini ku- single out (huwezi kusema) kwamba nani aliukubali au aliukataa, ninajua waliokuwa wanaupinga lakini siwezi kusema ni nani kwa sababu ilikuwa ni siri, uamuzi wa Baraza la Mawaziri ni siri,” 
alisema Diallo.

Septemba mwaka jana, Lowassa alinukuliwa katika vyombo vya habari akieleza kwamba wakati alipopendekeza mradi huo wa maji kwenye Baraza la Mawaziri wakati wa enzi ya Mkapa, ni mawaziri wawili tu ndiyo waliomuunga mkono.

Akizungumza katika Kanisa la AICT mjini Kahama, Shinyanga, Lowassa alinukuliwa akiwataja mawaziri waliomuunga mkono kuwa ni Jakaya Kikwete ambaye alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakati huo na Muhammed Seif Khatib aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Muungano).




Katibu mwenezi mkoa wa Shinyanga ndugu Emmanuel Mlimandago


Posted By Unknown23:15

Monday 22 September 2014

JOB OPPORTUNITIES AT TANZANIA BROADCASTING CORPORATION (TBC)

Filled under:

TANZANIA BROADCASTING CORPORATIONThe Tanzania Broadcasting Corporation (TBC) is a Public Service Broadcasterestablished by Government Order in 2007 and became operational on the 1stof July 2007 replacing the then Tanzania Broadcasting Services – TaasisiyaUtangazaji Tanzania (TUT). TUT was established in the year 2002 pursuant to Public Corporation Act No 2 of 1992, Government Notice No 23 of 14th June 2002. Its formation was a result of a merger of Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD) which was established in 1972 and TelevisheniyaTaifa (TVT) which was established in 1999.

Tanzania Broadcasting Corporation (TBC) invite applications from suitably qualified Tanzanians to fill the following posts:

  1. TECHNICIAN II                                                        -           33 POSTS (for Regional Transmitters)

QUALIFICATIONS:
Holder of Secondary Education Certificate plus Trade Test II / III or its equivalent from a recognised Institution. Computer skills are an added advantage.
DUTIES AND RESPONSIBILITIES:
  1. Carry out technical operations,
  2. Carry out  servicing and maintenance work of technical equipment,
  3. Ensure proper maintenance of all equipment at his/her workplace,
  4. Perform any other related duties as may be assigned by the supervisor.
Salary:
Within the Salary Scale of PGSS 5
  1. JOURNALIST II:                                                      -           2 POSTS
QUALIFICATIONS:
Holder of Bachelor Degree or Advanced Diploma in Journalism, Mass Communication, TV/Film Production
from a recognized Institution. Knowledge in word processing, graphics, photographing, photo-editing and video shooting is an added advantage. Computer skills are essential.
DUTIES AND RESPONSIBILITIES:
  1. Gather and write news and stories,
  2. Writes scripts and continuities and prepares programmes for radio and television products,
  3. Collects, reports and comments on news and current affairs for broadcasting by radio or television,
  4. Interviews politicians and other public figures at press conferences and on occasions, including individual interviews recorded for radio or television,
  5. Writes editorials and selects, revises, arranges and edits submitted articles and other materials for broadcasting on radio or television,
  6. Writes advertising copy promoting particular products or services,
  7. Selects, assembles and prepares publicity materials about business or other organizations for being broadcast through radio, television or other media,
  8. Provides professional and technical support to other junior reporters/journalists,
  9. Perform any other related duties as may be assigned by Supervisor.
Salary:
Within the Salary Scale of PGSS 10
  1. Records Management Assistant II                                             - 1POST
QUALIFICATIONS:
Holder of Advanced Certificate of Secondary Education (ACSE) or Certificate of Secondary Education (CSE) with pass in Kiswahili and English language and certificate in Records Management or its equivalent from a recognized Institution.  Computer skills are essential.
DUTIES AND RESPONSIBILITIES:
-           Receives files, deliver to the appropriate officer and collects and returns them to registry,
-           Opens relevant files according to record keeping regulations,
-           Keeps record of movement of files according to laid down procedures,
-           Traces, locates and retrieves files when needed by officers,
-           Receiving and register all official documents brought in the registry.
-           Arranging documents and files in ranking or cabinets in the registry.
-           Filing documents in the appropriate files.
-           Record and arrange efficient and timely dispatch of all correspondences
-           Perform any other related duties as may be assigned by the supervisor. Salary:
Within the Salary Scale of PGSS 5-6
  1. Procurement Management Officer II                                         -           2POSTS
QUALIFICATIONS:
Holder of Bachelor Degree or Advanced Diploma in Materials Management or its equivalent from a recognised  Institution and registered with Procurement and Supplies Professionals and Technicians Board (PSPTB).  Computer skills essential are essential. DUTIES AND RESPONSIBILITIES:
-           Provides support in placing orders for goods requested by user departments,
-           Inspects goods supplied to ascertain conformity to approved standards specifications and quality,
-           Follows up overdue orders,
-           Prepares monthly, quarterly, mid-year and annual stock report,
-           Clears goods imported by the Corporation,
-           Perform any other related duties as may be assigned by the supervisor.
Salary:
Within the Salary Scale of PGSS 10-11
 
  1. ICT Officer II                                                                         -           1 POST
QUALIFICATIONS:
Holder of  Bachelor Degree in Computer Science, Information Technology, Electronics or its equivalent from a recognised Institution.
DUTIES AND RESPONSIBILITIES:
-           Initiates development of information systems,
-           Assists in setting up and maintains servers, workstations and peripherals
-           Carries out system back-up and periodically tests recovery procedures.
-           Appraises the supervisor on release of updates and software,
-           Assists in providing IT support services to users,
-           Perform any other related duties as may be assigned by the supervisor. Salary:
Within the Salary Scale of PGSS 11-12
 
  1. Human Resource and Administrative Officer II                      -           1 POST
QUALIFICATIONS:
Holder of Bachelor Degree in Human Resources Management, Public Administration, Business Administration, Sociology or its equivalent from a recognized Institution. Computer Skills are essential. DUTIES AND RESPONSIBILITIES:
-           Assist in salary administration, remuneration scheme and management of Pension and terminal benefits,
-           Assist in the preparation of staff records regarding, staff leave and staff welfare,
-           Keep an update registers for staff position, disposition, engagements, confirmations and promotions,
-           Promote good industrial relations in the workplace,
-           Assist in management of the Pension scheme,
-           Participate on assessing training needs of personnel,
-           Collecting, keeping and updating personnel data and information.
-           Interpreting and implementing Scheme of Service.
-           Collecting, analysing and planning proper statistics records for human resources plans.
-           Preparing and handling seniority list.
-           Drafting internal circulars, letters and internal memorandum for official use.
-           Perform any otherrelated duties as may be assigned by the supervisor. Salary:
Within the Salary Scale of PGSS 10-11
  1. Estate Management Officer II                                          -           1POST
QUALIFICATIONS:
Holder of Bachelor Degree or an Advanced Diploma in Estate/Land Management and Valuation,  Architecture, Building Economics or its equivalent from a recognized Institution. Computer Skills are essential. DUTIES AND RESPONSIBILITIES:
-           Carries out periodic inspection of the Corporation’s buildings and assesses maintenance requirements,
-           Maintains an up to date record of real estates and assets register,
-           Provide support on following up procurement of Title Deeds for TBC properties,
-           Produces periodic reports on the status of TBC properties,
-           Prepares sketches and plans needed for making minor alterations to buildings and equipment.
-           Assists in innovative approaches to conditioning, maintaining and upgrading of the surroundings of the Corporation’s buildings.
-           Perform any other related duties as may be assigned by the supervisor. Salary:
Within the Salary Scale of PGSS10-11  
  1. Soundman II                                                                                    -           1POST
QUALIFICATIONS:
Holder of Diploma in Sound Recording or its equivalent from a recognised Institution with good command of Swahili and English language. Computer skills are essential.  DUTIES AND RESPONSIBILITIES:
-           Recording sound and music on location and in the studio with optimum sound quality and effects,
-           Deal with all sound transfers as may be requested by the producer,
-           Perform integration of music into the broadcast,
-           Ensure proper maintenance and operation of all sound recording devices,
-           Ensure optimum quality of sound at recording/dubbing sessions and proper blending of sound effects with music tracks into single cohesive unit,
-           Perform any other related duties as may be assigned by the supervisor. Salary:
Within the Salary Scale of PGSS 5-6
  1. DRIVER II                                                                              -           2  POSTS
QUALIFICATIONS:
Holder of Certificate of Secondary Education with passes in Kiswahili and English. Must have a valid class C driving license and Trade Test Grade III from a recognized Institution with driving experience of 2 years with accident free record. DUTIES AND RESPONSIBILITIES:
  1. Drive the Corporation’s vehicles towards approved destinations and in accordance with traffic regulations,
  2. Undertake minor mechanical repairs,
  3. Take vehicles due for routine maintenance/repair to the appointed service agents,
  4. Maintain motor vehicle log books,
  5. Make pre-inspection to the assigned vehicle at all times,
  6. Ensure that valid documents and permits are acquired prior commencement of any journey
  7. Report promptly accidents or incidents involving the vehicles to the relevant authority,
  8. Ensure that the vehicle assigned to him/her is maintained, serviced regularly and kept clean,
  9. Maintain a logbook and record all vehicle movements as instructed,
  10. Perform any other related duties as may be assigned by the supervisor.
Salary:
Within the Salary Scale of POSS 5

GENERAL CONDITIONS:
  1. All applicants must be citizens of Tanzania and not above 45 years old.
  2. Applicants must attach an up-to-date current curriculum Vitae (CV) having reliable contact, postal address, e-mail and telephone numbers.
  3. Applicants should apply on the strength of the information given in this advertisement.
  4. The title of the position applied for should be written clearly in the subject of the application letter and also marked on the envelope; short of which will make the application invalid.
  5. Applicants must attach their detailed relevant certified copies of all required academic certificates:
  6. Postgraduate/Degree/Advance Diploma/Diploma/Certificates.
  7. Postgraduate/Degree/Advance Diploma/Diploma/Transcripts.
  8. Form IV and Form VI National Examination Certificates.
  9. Computer Certificates.
  10. Professional certificates from respective boards.
  11. One recent passport size picture and birth certificate.
  12. FORM IV AND FORM VI RESULT SLIPS ARE STRICTLY NOT ACCEPTED
  13. Testimonials, Partial transcripts and results slips will not be accepted.
  14. Presentation of forged academic certificates and other information in the CV will necessitate to legal action
  15. Applicants for entry levels currently employed in the Public Service should not apply, they have to adhere to Government Circular Na. CAC. 45/257/01/D/140 dated 30th November, 2010.
  16. Applicants should indicate three reputable referees with their reliable contacts.
  17. Certificates from foreign examination bodies for Ordinary or Advanced level Education should be certified by The National Examination Council of Tanzania (NECTA).
  18. Certificates from foreign Universities should be verified by The Tanzania Commission for Universities (TCU)
  19. Deadline for application is two weeks from the 1st day of advertisement.
  20. Applicants with special needs/case (disability) are supposed to indicate
  21. Women are highly encouraged to apply
  22. Only short listed candidates will be informed of a date for interview
  23. Application letters should be written in English.
APPLICATION LETTERS SHOULD BE POSTED TO THE FOLLOWING ADDRESS.
Director General,
Tanzania Broadcasting Corporation,
P.O. Box 9191,
Dar es Salaam.

source: www.tbc.go.tz/kazi

Posted By Unknown00:35

JOB OPPORTUNITIES AT THE ST.AUGUSTINE UNIVERSITY OF TANZANIA (SAUT)

Filled under:

The St. Augustine University of Tanzania (SAUT) is a private higher learning Institution Owned by Tanzania Episcopal Conference (TEC) with a vision of holistic development of a person and respect of human dignity.
SAUT is an equal opportunity employer and it intends to recruit competent academicians capable to impart professional skills and inculcate civic and social values to students that will make them better citizens. The applicants are required to fill the following vacant positions:-

1.0 Assistant Lecturer
1.1 Language and Linguistics (2 posts)
1.2 Education Foundation (5 posts)
1.3 Kiswahili (2 post)
1.4 History (2 posts)
1.5 Geography (2post)
1.6 Literature (3 posts)
1.7 Tourism (2 posts)
1.8 Hospitality (2 posts)
1.9 Marketing (2 posts)
1.10 ICT (2 posts)

2.0 Entry qualification for Assistant Lecturer post

  • Master degree  in relevant field from the reputable higher learning Institution at 4.0 and above GPA
  • Holder of relevant of bachelor degree or Equivalent from reputable Higher academic Institution  ( First class, or Upper second class, with GPA 3.8 or a B+ in relevant subjects for unclassified degree.
2.1 General attributes
  • Language proficiency
  • Ability to communicate information, knowledge and skills to others
  • Ability to prepare and deliver own teaching materials
  • Problems solving and innovation skills
  • Ability to recognize those having difficulties, intervene, and provide help and support
  • Ability to prepare quality research proposals
  • Motivation for Innovation, further Learning and Continuing professional development 
3.0   Lecturer
3.1   Language and Linguistics (1 post)
3.2   Education Foundation  (2 posts)
3.3   Geography (2 post)
3.4   Literature (2 posts)
3.5   Tourism (2 posts)

4.0 Entry qualification for Lecturer’s post
  1. PhD degree in the relevant field with a master degree at 4.0 GPA from reputable Higher Learning Institutions registered/recognized by TCU.
4.1 The general attributes
  • Ability to design, set, administer and supervise different assessment items
  • Ability to mark student scripts and course work assessment items and provide feedback
  • Ability to prepare and deliver own teaching materials
  • Ability to carry out independent research and provide feedback
  • Ability to supervise research and other knowledge and skills development activities.
5. Terms of Employment
Successful candidates will be employed on Contract terms of three (3) years however the confirmation shall be made after satisfactory completion of first year.

6. Remuneration
Attractive remuneration package will be offered to successful candidates

7. Mode of Application
Application should be accompanied by the detailed Curriculum Vitae (CV), Providing names, positions and detailed contacts of three (3) Reliable referees and copies of relevant Certificates and Transcripts.

8. Deadline for Receiving Applications
The applications should be submitted to the address below not later than Thursday 2nd October 2014 at 1600 hours. Any application received after due date will not be considered.

Only shortlisted candidates will be contacted for interview. 
Applications should be addressed to
 Human Resource Director,
St. Augustine University of Tanzania,
P.O. BOX 307,
MWANZA.         


Email: paulgwaltu@yahoo.com

Source: http://www.saut.ac.tz/index2.php/employment-opportunities

Posted By Unknown00:25

Friday 12 September 2014

JINSI YA KUENDELEA KUWA MLIMBWENDE KIPINDI CHA UJAUZITO MPAKA KUJIFUNGUA

Filled under:



Kipindi cha ujauzito wanawake wengi hujikuta wakiacha kuzingatia hatua mbalimbali za kujitunza ili kubaki warembo, matokeo yake hupoteza mvuto.
Hali hiyo inaweza kuendelea hata baada ya kujifungua na huenda ikawa mbaya zaidi kwa kuwa mara nyingi kipindi hicho mama hujikuta akitumia muda mwingi kumwangalia mtoto.
Kujifungua au ujauzito haiwezi kuwa sababu ya mwanamke kupoteza urembo uliokuwanao awali. Hivyo ni jukumu la mwanamke mjamzito au aliyejifungua kuhakikisha anabaki na mvuto wake ukiwa kwenye kiwango stahiki.
Kuwa mrembo siyo lazima upake vipodozi vyenye kemikali kwani vinaweza kumsababishia madhara mtoto kwa kuwa atatumia muda mrefu akiwa mwilini kwako.
Katika kipindi hiki mama mjamzito au aliyejifungua anatakiwa kuepuka kupaka mafuta, losheni au manukato yenye harufu kali inayoweza kuwa na madhara kwa mtoto hata kumsabishia wakati mgumu katika kupumua.
Ni vyema utumie vipodozi visivyo na kemikali ili kujilinda usipoteze mvuto wako. Pia tumia muda mwingi kufanya mazoezi mepesi yatakayoweza kukusadia kutengeneza umbile (shape), yako na kuifanya ionekane yenye mvuto wa hali ya juu hata ikiwa umetoka kujifungua.
Hakikisha pia kucha zako zinakuwa fupi na safi, hii haimaanishi kwamba huruhusiwi kupaka rangi unaweza kuziremba kwa mtindo wowote unaopenda lakini ziwe katika kiwango ambacho hakitamdhuru mtoto kwa namna yoyote.
Kitu muhimu cha kuzingatia katika kipindi hicho ni usafi na mwonekano wa ndani na nje. Kwa kufanya hivyo, hata mtoto atakuwa katika mazingira salama yanaweza kumtamanisha mtu mwingine kutaka kumshika.

Posted By Unknown08:35

SITTA ASHAMBULIWA KAMA MWEWE

Filled under:


Samuel Sitta
Mpango wa Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta wa kutaka ya wajumbe wake walioko nje ya nchi kupiga kura kupitisha Katiba inayopendekezwa, umepingwa na wasomi, ukielezwa ni kinyume na kanuni za Bunge na sheria za nchi.

Wasomi hao, wanaharakati na wanasiasa wamesema Tanzania haina utaratibu wa raia wake kupiga kura wakiwa nje ya nchi na kwamba hiyo ni mbinu ya kufanya udanganyifu.
Juzi, Sitta alisema wajumbe wa Bunge hilo watakaokuwa nje ya nchi kwa sababu zozote, ikiwamo ya matibabu na Hijja, watapiga kura hukohuko mara upigaji kura utakapoanza Septemba 26, mwaka huu na kuwataka wajumbe hao kuacha mawasiliano yao watakapokuwa nje na kwamba uongozi wa Bunge umeanza kufanya mawasiliano na balozi mbalimbali za Tanzania, ili wawepo watumishi wake watakaokula kiapo cha kisheria kusimamia kazi hiyo.
Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana alisema suala la Watanzania kupiga kura wakiwa nje ya nchi halimo kwenye kanuni zinazoongoza Bunge hilo na ni vizuri utaratibu huo ukaachwa.
Alisema anachokiona sasa ni Bunge kuendelea kupoteza fedha za wananchi wakati hakuna maridhiano huku uamuzi ukiwa umefikiwa kwamba Katiba Mpya itapatikana baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alisema: “Hata kanuni za mabunge ya Jumuiya za Madola ambazo sisi tunazifuata ikitokea mjumbe anaumwa anapelekwa kwenye ukumbi wa Bunge kupiga kura, kura haipigwi sehemu yoyote.
“Hata katika Bunge la Uingereza ikionekana mjumbe anatakiwa kupiga kura lakini anaumwa atapelekwa ukumbini kwa msaada wa uongozi wa Bunge, ili aweze kutimiza haki yake ya kidemokrasia lakini haki hiyo haiwezi kumfuata huko aliko.
“Sitta analichukulia suala la Katiba kama lake binafsi, utaratibu wa kupiga kura za kificho haukubaliki kwa sababu utasababisha uchakachuaji,” alisema.
Mkurugenzi Mkuu wa Utetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Onesmo Olengurumwa alisema Tanzania haina utaratibu wa raia wake kupiga kura wakiwa nje ya nchi.
Mwanasheria huyo alisema kinachofanywa na Sitta kinaonyesha namna Bunge la Katiba linavyolazimisha mchakato huo.
“Kituo pekee cha wajumbe wa Bunge Maalumu kupiga kura ni ndani ya Ukumbi wa Bunge na si vinginevyo. Kinachofanywa na Sitta ni kuwahadaa Watanzania, mtu anaumwa atapigaje kura wakati hata kwenye majadiliano hakuwapo? Unalipigia kura jambo ambalo umeshiriki kwenye majadiliano,” alisema.

Alisema Tanzania haina utaratibu wa raia wake kupiga kura wakiwa nje ya nchi na kwamba endapo Serikali inataka kuuruhusu basi ifanye hivyo.

Posted By Unknown04:33

MWANAUME APATA HISIA ZA UJAUZITO

Filled under:

Harry Ashby ni mwanaume wa kwanza nchini Birmingham kupata ruhusa ya kupumzika nyumbani baada ya kusumbuliwa na homa mithili ya mwanamke mja mzito.

 
Harry Ashby ameripotiwa kuwa na dalili za ujauzito kama mchumba wake
Amekuwa akipatwa na homa za vipindi hasa nyakati za asubuhi baada ya mchumba wake aitwae Charlotte kuwa mjamzito, mtandao wa Itv news umeeleza.

Habari zinasema mwanaume huyo mwenye miaka 29 anayefanya kazi ya ulinzi ,amesema ameongezeka uzito na tumbo limekua mithili ya aliye mjamzito na kudai kuwa anasumbuliwa na maumivu ya mgongo na cha ajabu amekuwa na hamu ya baadhi ya vyakula.

Harry ameripotiwa kuwa na dalili za kuwa mja mzito miezi miwili baada ya kubaini kuwa mchumba wake ni mjamzito.

Harry amekuwa akipatiwa dawa na inasemekana anaweza kudai mafao wakati akiwa katika mapumziko hayo.

Posted By Unknown04:03

OSCAR PISTORIUS ASUBIRI HUKUMU BAADA YA KUUA BILA KUKUSUDIA

Filled under:

 
OSCAR PISTORIUS
Jaji wa mahakama kuu ya Afrika Kusini Thokozile Masipa anaendelea hii leo kutoa hukumu yake dhidi ya kesi ya mauaji inayomkabili mwanariadha wa Olimpiki Oscar Pistorius huko Afrika Kusini.

Tayari amemuondolea makosa ya mauaji, na badala yake Pistorious anakabiliwa na makosa ya kuua bila kukusudia.

Katika uamuzi wake huo wa kumuondolea Mwanariadha Oscar Pistorius mashtaka ya mauaji ,jaji Thokozile Masipa alisema mwendesha mashtaka hakuthibitisha kesi yake pasi na shaka yoyote.
Hata hivyo itabainika vyema baadae leo iwapo atapatikana na hatia ya mauji pasi na kukusudia wakati jaji atapoitolea kesi hiyo hukumu yakini.

Pistorius amekana mashtaka ya kumua aliyekuwa mpenzi wake Reeva Steenkamp hapo mwaka jana katika siku ya wapendao Valentine day pale alipomfyatulia risasi kumuua.
Mwendesa mashtaka amekuwa akisisitiza kuwa Pistorius alimpiga risasi Reeva wakati wa ugomvi baina yao lakini Pistorius amekuwa akijitetea kuwa alidhani ni mwizi aliyevamia nyumba yake.

Jaji amesema wakati wa tukio hilo Pistorius alikosa makini kwa kutumia bunduki yake vibaya.

Mwandishi wetu wa Afrika kusini anasema uamuzi huu wa awali umewashangaza wengi waliokuwa wakifuatilia kesi hii kwa karibu wakisema inavyoelekea anaweza kupewa kifungo chepesi.

Anaepatikana na hatia la Kosa la kuuwa bila kukusudia hupewa kifungo kisichozidi miaka kumi na tano jela na pia kuna uwezekano wa kutumikia baadhi ya mda huo kifungo cha nje.
Hata hivyo mbali na uwezekano wa rufaa baada ya hukumu anakabiliwa pia na shtaka la matumizi mabaya ya bunduki

Posted By Unknown03:57

MSIKITI WA MTAMBANI KINONDONI WAUNGUA MOTO KWA MARA NYINGINE

Filled under:



 
AMSIKITI WA MTAMBANI  KINONDONI


Habari zilizotufikia hivi punde Msikiti wa Mtambani uliyopo Kinondoni jijini Dar es Salaam unateketea kwa moto hivi sasa. Hii ni mara ya pili msikiti huo kutetekea kwa moto baada ya kuungua Agosti 13 mwaka huu. Habari zaidi zitawajia hivi punde.

Posted By Unknown03:44

Sunday 7 September 2014

TAARIFA YA BENKI KUU KUHUSU TOLEO LA SHILINGI MIA TANO MPYA

Filled under:

Mkurugenzi Huduma za Kibenki kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Bw. Emmanuel Boaz (kulia) na Mshauri wa Fedha kutoka ofisi hiyo Bw. Hassan Jarufu wakiwaonesha waandishi wa Habari(Hawapo Pichani) Toleo jipya la sarafu ya Shilingi 500 inayotarajiwa kuingizwa kwenye mzunguko kuanzia mwezi Oktoba 2014.
(picha: Hassan Silayo/Maelezo)
 Benki Kuu ya Tanzania ndiyo chombo chenye jukumu la kutoa sarafu na noti halali (legal tender) zinazotumika nchini. Katika kutekeleza jukumu hili Benki Kuu hutengeneza noti na sarafu zenye uwiano mzuri wa thamani (denominations) unaozingatia uwezekano wa zile zenye thamani kubwa kuweza kugawika katika zile zenye thamani ndogo ndogo.

Hii hulenga kurahisisha upatikanaji wa chenji na uwezekano wa wahitaji wa viwango mbalimbali vya bidhaa na huduma kupata katika mafungu yatakayokidhi mahitaji yao.
Katika kutekeleza jukumu hili, Benki Kuu imetoa toleo jipya la Sarafu ya Shilingi 500. Hatua hii imezingatia yafuatayo:
  • Kwamba noti ya shilingi mia tano (500), ndiyo inayotumika zaidi kwenye manunuzi ya kawaida ya kila siku ya wananchi wengi kuliko noti nyingine yoyote. Hivyo noti hiyo hupita kwenye mikono ya watu wengi katika kipindi cha muda mfupi sana na kuchakaa haraka.  
  • Noti hizi hukaa katika mzunguko kwa muda mrefu bila kurejeshwa kwenye mabenki kwa wakati muafaka ili zibadilishwe zinapokuwa zimefikia ukomo wake.
  • Sarafu hukaa kwenye mzunguko kwa miaka mingi zaidi kuliko noti.
Sarafu hii inatambuliwa kwa kuangalia yafuatayo:
  • Umbo lake ni la duara lenye michirizi pembezoni, kipenyo cha milimita 27.5 na uzito wa gramu 9.5 
  • Ina rangi ya fedha na imetengenezwa kwa madini aina ya chuma (Steel) na “Nickel” 
  • Kwa mbele ina sura ya Rais wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Sheikh Abeid Aman Karume na kwa nyuma ina taswira ya mnyama nyati akiwa mbugani.
  • Ina alama maalum ya usalama iitwayo “latent image” iliyopo upande wa nyuma ambayo ni kivuli kilichojificha. Kivuli hiki huonesha thamani ya sarafu ‘500’ au neno ‘BOT’ inapogeuzwa-geuzwa.
Sarafu hii mpya ya shilingi mia tano (500) inatarajiwa kuingizwa kwenye mzunguko kuanzia mwezi Oktoba 2014.
Sarafu hii, itakuwa ikitumika sambamba na noti zilizopo sasa za shilingi mia tano mpaka hapo noti hizo zitakapokwisha katika mzunguko.
Pamoja na taarifa hii; tunawaomba wananchi kuendelea kufuatilia vipindi mbalimbali vitakavyokuwa vinaeleza jinsi sarafu hii ilivyo na namna ya kutunza noti na sarafu zetu kwa njia salama.
 
Ahsanteni Sana

Posted By Unknown09:44

DK KINGWANGALLA ATANGAZA NIA YA KUWANIA URAIS 2015

Filled under:

Ndugu viongozi mlioko hapa, wageni waalikwa, wanahabari na watanzania wenzangu mnaonisikiliza;
Ni heshima kubwa sana kwangu kupata fursa hii. Ni katika nchi chache sana duniani, mtoto wa maskini kama mimi, aliyewahi kutembea mitaani akiuza karanga, Big G, maandazi, jerebi na samaki ili kusaidia wazazi kupata chochote kwa ajili ya kulisha familia anaweza kuota kuwa Rais wa nchi yake. Kwamba, mtoto aliyeenda shule bila viatu anaweza kuwa Daktari. Hii inamaanisha misingi ya haki na usawa kwa wote iliyowekwa na waasisi wa Taifa hili haikuwa ndoto za alinacha, bali ukweli na uhalisia, na inafanya kazi. Kwamba, siyo lazima uwe mtoto wa tajiri ndiyo uoneshe kipaji chako.

Hili peke yake linanipa sababu ya ziada ya kwa nini nitamani kuota kuwa Rais – nataka niwe mfano hai wa mafanikio ya Ndoto ya waasisi wa Taifa letu, kuwa sote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tuna
haki na fursa sawa bila kujali nani anatokea familia ipi. Hii ni Tanzania ya ndoto za waliotutangulia. Ni lazima atokee kiongozi wa kizazi hiki anayetamani kuiongoza Tanzania itakayodumu kwenye misingi hii: kwamba sisi sote ni ndugu, na tuna fursa sawa. Kwamba, kuendelea kimaisha na kibinafsi ni haki ya binadamu na si hisani. Kwamba, mtoto wa mama ntilie kama nilivyokuwa mimi hapa, ana haki na fursa ya kuwa mbunge ama Rais wa nchi, sawa kabisa na mtoto wa Mbunge.

Kwa namna ya kipekee nichukue fursa hii kuwashukuru na kuwapongeza waasisi wa Taifa letu kwa kusimamia tunu hizi. Niwashukuru pia viongozi wote walionitangulia kwa kuzilinda, na niahidi nitakuwa wa mwisho kuisaliti nchi yangu kwenye mambo haya.

Leo nimefika hapa kwa sababu chama change kina mfumo mzuri ulioasisiwa na Mwl. Nyerere na umelindwa na Wenyeviti waliomfuatia mpaka na sisi tumeukuta. Leo nimefika hapa kwa sababu Rais Jakaya Kikwete na wajumbe wenzake wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu walitumia misingi imara iliyowekwa na waasisi wa Chama changu kuamua kuwa nami nina haki ya kuwa Mbunge. Leo nazungumza hapa nikiamini kuwa ni misingi hiyo hiyo itatoa uongozi wa Taifa letu katika awamu ijayo.

Babu yangu Kizaa Baba aliishi Kijijini Goweko, Mlimani, na alikuwa mfugaji mkubwa wa ng’ombe na mrina asali mashuhuri. Yeye na mkewe waliishi maisha ya heshima sana pale kijijini. Hawakuwahi kusoma wala kuajiriwa japokuwa Babu yangu aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali ndani ya Chama Cha TANU na baadaye CCM katika ngazi ya Kata.

Babu yangu na Bibi yangu kizaa mama waliishi Nzega, na ndiyo walionilea baada ya ndoa ya mama yangu na baba yangu kuvunjika. Walinifundisha mambo mengi, kubwa likiwa ni kujiamini, pia kufanya mambo yangu kwa bidii, uadilifu, umakini na kwa nidhamu ya hali ya juu. Bibi yangu huyu hakusoma shule ya kizungu japokuwa alijifunza kusoma na kuandika. Babu yangu alikuwa mjukuu wa Chifu na hivyo alipata fursa ya kusoma Tabora School miaka miwili mbele ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere. Alifanya kazi mbalimbali chini ya serikali ya wakoloni, na alishiriki harakati za kuanzishwa na kusambaa kwa chama cha TAA na baadaye TANU. Babu yangu aliamini kuwa “binadamu wote ni sawa na kwamba kila mtu anastahili kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake”, na kwamba ukoloni haukuwa kitu cha sawa, na hivyo kujitawala wenyewe dhidi ya wazungu ilikuwa ni haki yetu; pia aliamini katika elimu, na hivyo alifanya juhudi kusomesha mabinti zake watatu, mama yangu aliishia kwenye ualimu kabla ya kuingia kwenye ndoa. Babu aliamini kuwa Tanzania ya mabinti zake itahitaji wasomi, ndoto ambayo ninaishi kuitekeleza kwa ajili ya mabinti zangu wawili na Kaka yao, HK Jr.

Japokuwa bibi na babu yangu wameishatangulia mbele ya haki, naamini wananitazama na kutabasamu huko waliko.

Ninaishi nikiamini kuwa hadithi ya maisha yangu ni mfano hai kwa maisha ya watanzania wengi. Na kwamba, nina deni la kulipa kwa vizazi vijavyo kwa kuwa mimi ninafaidi matunda ya mti uliopandwa na vizazi vilivyonitangulia. Naliona jukumu la kuhakikisha vizazi vijavyo vinafaidi urithi wa Tanzania kuwa ni la kwangu na wenzangu wa kizazi hiki.

Kazi yangu imenifikisha sehemu nyingi sana za nchi yetu – vijijini na kwenye majiji, imenikutanisha na watu wa kila aina – matajiri kwa maskini, wazee kwa vijana – hakuna hata mmoja kati ya watu hawa anayetegemea Serikali itamtatulia kero zake zote. Wanajua wanapaswa kufanya kazi kwa bidii ili wasonge mbele – na wana nia ya kufanya hivyo.

Nenda kwa wafanyabiashara wakubwa kule Pugu Road viwandani, kwa watumishi pale hospitali ya Taifa Muhimbili, ama pale sokoni Kariakoo kwa wafanyabiashara, wote watakuambia hawapendi kuona kodi zao zikitafunwa na wachache pale TRA, ama kulipa posho za bure kwa wabunge na mawaziri kule Bungeni, kulipia mashangingi ya viongozi na watendaji, kulipia tiketi za ndege daraja la kwanza kwa ajili ya safari za viongozi na wataalamu wetu kwenda kujifunza kupambana na umaskini wakati wakirudi wanauacha uzoefu uwanja wa ndege, ama kulipia semina, warsha na makongamano ya wataalamu ya kuandika sera za MKUKUTA, MKURABITA na kuandaa bajeti zisizotekelezwa kila mwaka.

Watanzania wanataka kupata huduma bora za afya, elimu, maji, miundombinu.
Nenda kule kwa watani zangu, Nanyumbu, ama Tandahimba, ama kwa ndugu zangu kule Nduli, Kyela, wazee kule watakuambia hawategemei Serikali itawaletea ubwabwa kwenye sahani za fedha, wanajua Serikali haitowafanyia kila kitu, lakini wanajua kabisa kuwa wanapaswa kufanya kazi kwa bidii na wamekuwa wakifanya hivyo siku zote. Wanachohitaji wao ni kujengewa mazingira wezeshi kushiriki shughuli zao za kilimo ama biashara, waelekezwe namna ya kuongeza uzalishaji kwa kutumia njia za kisasa za kilimo chenye tija na ufanisi, waelekezwe wanapataje pembejeo, wanapataje mikopo yenye riba nafuu, wanahitaji, mwisho wa siku, wajue wapi watauza mazao yao kwa uhakika na bila kudhulumiwa wala kucheleweshewa malipo.

Watu hawatarajii serikali itabeba mizigo yao yote. Lakini wanaamini kabisa, kwamba tukibadili kidogo tu vipaumbele vyetu, tukibadili namna tunavyoendesha serikali, tukibadili kidogo namna tunavyoendesha uchumi wetu, tutaweza, kwa kiasi kikubwa, kubadili muelekeo mzima wa maisha ya baadaye ya watoto na wajukuu zetu. Tutatoa uhakika wa kuiondoa nchi yetu kutoka miongoni mwa nchi maskini kabisa duniani.

Na mimi, kama watanzania wenzangu wengi, nina imani kubwa kabisa, kwamba tunaweza kubadili mustakabali wa Taifa letu. Tunaweza kufungua milango ya maisha bora zaidi kwa watanzania. Tutatoa fursa sawa kwa kila mtanzania kuishi kwa matumaini, kwamba atabadili maisha yake wakati wowote ule kuanzia leo. Tutaweza kuamsha ari ya kila mtanzania kuongeza bidii kwenye kazi akitumaini na kuamini kuwa kesho yake itakuwa bora kuliko jana yake, kuwa naye ataishi kwa heshima, raha na starehe ndani ya nyumba yake.

Ninaamini, kutokea ndani kabisa ya mifupa yangu, kuwa tukifanya uchaguzi sahihi wa vipaumbele vyetu, tukibadili namna tunavyoendesha serikali yetu, haya ninayoyasema si ndoto za mchana. Ni mambo yanayowezekana.

Watanzania wengi wanaamini, kuwa tukifanya uchaguzi sahihi wa vipaumbele vyetu, mabadiliko makubwa, na ya haraka yatatokea kwenye uchumi wetu. Wanaamini tukichagua kiongozi sahihi mwakani, anayejua mahitaji ya nchi yetu kwa sasa na baadaye, tutafanikiwa.

Nyote mliopo hapa na wanaotusikiliza kutokea nje ya hapa mna jukumu la kututazama kwa ukaribu sana, kututathmini na kutupima sote; tuliojitokeza hadharani, walioanza safari za matumaini, wanaotajwa tajwa, na wale wanaosubiri kuoteshwa ili wakati muafaka ukifika muwape taarifa sahihi watanzania, kuwa kati yetu sote, ni nani anafaa kutuongoza kuelekea Tanzania ya ndoto zetu!

Kuwa, ni nani kati yetu ataweza kuwa Amiri-jeshi-mkuu, siyo kwa uanajeshi wake bali kwa uwezo na utayari wake wa kuwashirikisha wataalamu wa majeshi na kuamua kwa busara kutumia nguvu za kijeshi pale inapolazimika baada ya kupima na kuchambua aina nyingine zote za kutafuta suluhu za migogoro kabla ya kuamua vita.

Kuwa, ni nani kati yetu anayeamini katika uhuru, haki na usawa na wajibu wa watu wote, kama unavyolindwa na Katiba, anayeamini katika haki ya kuabudu lakini asiyekuwa tayari kuitumia haki hiyo kuwagawa watanzania kutokana na dini zao.

Kuwa, ni nani kati yetu anayeamini katika Haki ya kupata huduma bora za afya, elimu, maji, kama wanavyopata wabunge na mawaziri wetu, kama wanavyopata mahakimu na majaji wetu, kama wanavyopata wafanyabiashara na wakurugenzi wetu.

Kuwa, ni nani kati yetu ataweza kuhakikisha kuwa watanzania wote wanapata haki hizi bila kutazama hali zao kiuchumi ama daraja zao kijamii.

Kuwa, ni nani kati yetu anaamini zaidi katika uhuru na kujitegemea kwenye masoko na malighafi ili kudhibiti uchumi wetu mpana wa ndani, kujitegemea kwenye masoko ya pamba na nguo, kwenye mafuta ya kula, kwenye chakula cha uhakika kwa ajili ya watu wetu, kwenye mafuta na gesi ili tukwepe mtego wa kuwa sehemu ya uchumi, masoko na biashara za hasara na faida za makampuni makubwa ya kimataifa nje ya mipaka yetu. Ili tulinde thamani ya fedha yetu, ili tuwe na uhakika wa ustawi wa maisha ya watu wetu ndani ya nchi bila athari kubwa kutoka nje ya nchi yetu.

Kuwa, ni nani miongoni mwetu anaakisi taswira sahihi zaidi ya watanzania walio wengi, historia yake, rekodi yake, wajihi wake, mtazamo wake, ndoto zake, zinaakisi ‘utanzania’ halisi. Kuwa, yeye ni hitaji sahihi la watanzania.

Wakati ukifika, muwaeleze watanzania ukweli, wafanye uamuzi unaotokana na taarifa sahihi, wachague mtu sahihi.

Mimi, Ndugu zangu, natangaza rasmi sasa, kuwa ninatia nia ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2015.

Na nimefikia uamuzi huu bila kuelekezwa, kusukumwa, kushawishiwa, kupangiwa ama kupanga na mtu ama na kikundi cha watu, bali kwa utashi na utayari wangu. Na ninayasema haya, haswa baada ya kutafakari mambo mengi kwa kina: mahitaji ya sasa na baadaye ya Tanzania ya ndoto zangu, uwepo wa fursa ya kugombea na kushinda uchaguzi ujao, uwezo wangu wa kuchambua mambo, kutafakari, kufanya maamuzi sahihi, kuchukua hatua za utekelezaji na kusimamia utekelezaji, uadilifu na uzalendo wangu, na zaidi nia yangu ya kuwa sehemu ya watanzania wengi tunaotaka kuona mapinduzi ya kifikra katika nchi yetu – mapinduzi ambayo yatatia chachu ya mabadiliko ya namna tunavyochagua vipaumbele vyetu kama Taifa na namna tunavyosimamia utekelezaji wa mambo mazuri tunayojipangia kama Taifa.

Ninatangaza nia ya kugombea Urais nikiwapa fursa watanzania wanipime na kunitazama mwenendo na uwezo wangu, nikiamini kabisa nitapimwa na kuungwa mkono ama kutoungwa mkono si kwa rangi ya ngozi yangu, si kwa jinsi yangu, si kwa umri wangu, na wala si kwa daraja langu kwenye jamii, dini yangu, ama kabila langu. Ninaamini nitapimwa kwa sifa na uwezo wangu, kama mtanzania.

Watanzania tuna sifa moja kubwa; kwenye mambo ya msingi ya kitaifa, tunakubaliana kuwa maslahi ya Tanzania hupanda juu ya maslahi yetu binafsi. Tudumishe utanzania wetu.

Ninaamini katika Ndoto ya Tanzania. Kuwa leo miaka 50 ya kuwa Jamhuri ya Tanzania tuna kila sababu ya kuwa Taifa la dunia ya kwanza, viongozi waliotutangulia wameandaa misingi ya kuifikisha Tanzania kwenye matamanio yetu. Kizazi chetu cha kina jukumu na wajibu wa kuikimbiza Tanzania kufikia kwenye ahadi inayotokana na ndoto za wazee na waasisi wa Taifa letu. Binafsi, niko tayari kulibeba jukumu hilo bila woga wala wasiwasi, maana naamini tusipojitokeza watu kama mimi, tutajikuta tunaongozwa na watu wasiostahili. Nina suluhu ya changamoto kubwa za leo na kesho: kupigana na njaa na kuhakikisha usalama wa chakula kwa watu wetu, tatizo la ajira kwa vijana na changamoto ya mabadiliko ya tabia nchi ni miongoni mwa mambo ambayo kizazi chetu kitapaswa kuyafanyia kazi kwa haraka na umakini wa hali ya juu.

Mimi ninaamini kwamba, kama hata mimi nimefika hapa, basi kila mtanzania anaweza, na ana haki ya kufika hapa na kwenda mbele zaidi yangu. Mafanikio siyo haki ya wachache, ni tunu ya Mwenyezimungu kwa kila mtu. Ninaamini ni haki ya kila mtanzania kuota ndoto yake, kuifanyia kazi na kuifikia. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ina wajibu wa kutoa fursa kwa watu wake kuota ndoto zao na kufikia mafanikio bila kukwama.

Na ndugu watanzania wenzangu, amini nawaambia, kuwa, mbele yetu tuna kazi ya ziada ya kufanya. Kazi ambayo ninaamini tunaiweza tukiamua; uwezo tunao, sababu tunazo na nia tunayo – sema tuna mapungufu makubwa kwenye kuchukua hatua za kutenda.

Mimi naamini kwamba; E Pluribus unum. Baina ya wengi, mmoja!

Kwamba; Mimi ni mmoja kati ya uwingi wetu. Siwezi kuwa salama kama wengine hawako salama, siwezi kuwa na raha kama wengine wanateseka. Ninaongozwa na ile dhana kwamba, matatizo ya mwenzangu, ni ya kwangu, na si yangu peke yangu, ni yetu sote kama jamii moja.

Hivyo:
- kitisho cha njaa ya familia fulani maskini kule Sakasaka, wilayani Meatu, ni kitisho changu na familia yangu, hata kama siyo familia yangu.

- Kucheleweshewa haki ya kuhukumiwa kwa mtuhumiwa wa mauaji ya kule Sombetini, ni kitisho kwangu pia, hata kama kesi siyo yangu.

- Mzee Makame wa kule Wete, Pemba, aliyefiwa na watoto wake akakosa msaada na yeye hana nguvu za kuzalisha tena, anavyokula mlo mmoja kwa siku ili asukume siku, inaniumiza na kunigusa moyoni, hata kama yeye siyo babu yangu.

- Mama John ni mpishi mzuri wa wali nazi kwa maharage, na ana wateja wengi mtaani kwake maeneo ya Mtaa wa Sikukuu, Sokoni Kariakoo; akifukuzwa, akapigwa virungu, akanyang’anywa pesa zake, akadhalilishwa na kumwagiwa chakula chake na mgambo wa jiji la Dar es salaam kwa kuwa anafanya biashara mahala pasiporuhusiwa, inaniumiza na kunigusa moyoni, hata kama yeye si mama yangu.

- Kama kuna mtoto asiyejua kusoma na kuandika kule Mrijo Chini kwa watani zangu warangi, hiyo inaniuma na kunigusa sana moyoni, hata kama yeye si mwanangu.

- Bwana Kalumanzila ni mmachinga nguo za mitumba mitaani. Yeye huchukua nguo zake kumi kwa kuaminiwa na mwenye belo kutokea soko la Karume, akiuza anachukua kifaida kidogo cha juu kinachozidi hapo juu na kurudisha pesa ya mwenye mali Karume jioni ya siku hiyo. Elfu mbili ama tatu anayopata inamfanya aishi yeye na mkewe na watoto wake. Akifukuzwa barabarani na akanyang’anywa mali, anakosa kazi ya kufanya na analazimika kumtumikia bosi mwenye mali mpaka atakapofidia mali iliyopotea bila kupata cha juu. Shida na madhila anayoyapata bwana Kalumanzila zinaniumiza na kunigusa sana moyoni, hata kama yeye si mjomba wangu.

Tarehe 4, Agosti 2014, Rais Kikwete akihutubia kwenye Kituo cha kimataifa cha maendeleo (Center for Global Development) alisema: “…Nataka na natamani kuwa Rais wa mwisho wa Tanzania kuongoza nchi masikini. Raslimali ya gesi inatoa nafasi na fursa kubwa kwa nchi yetu kuondokana na umasikini. Mimi nimeongoza nchi masikini, lakini nataka mrithi wangu kuongoza nchi yenye ustawi na utajiri…” Mimi nasema hivi: nataka na natamani kuwa Rais wa kwanza wa Tanzania kuongoza nchi Tajiri. Kama nitafanikiwa kuwa Rais, nitatumia miaka ya awali ya uongozi wangu kuikimbiza Tanzania kuelekea kwenye ndoto hii.

Mungu awabariki.
Mungu ibariki Tanzania.
Mungu ibariki Afrika.


Dk. Khamis Kigwangallah wakiigia katika chumba cha mkutano tayari kwa kuanza mkutano huo.


Dk Kigwangallah akitangaza nia yake ya kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania wakati alipokutana na waandishi wa habari, ambapo amesema hajasukumwa na mtu yeyote ila ni yeye mwenyewe ameamua kwa moyo wake.


Dk Kigwangallah akimtambulisha mke wake Dk Bayoum Awadh wakati wa mkutano huo.


Mzee Nasser Said Mussa, baba mzazi wa Dk. Kigwangallah na mama yake mzazi Mama Bagaile Lumola.



Mzee Nasser SAid Mussa baba mzazi wa Dk Kigwangallah na mama yake mzazi Mama Bagaile Lumola na watoto wake Sheila.


Mchungaji Patrick Saso akifanya maombi kabla ya kuanza kwa mkutano huo.


Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo.


Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo.


Sheikh Abubakary Mwita akiomba dua kabla ya kuanza kwa mkutano huo.

Picha: Habari Mseto blog



Dk Kigwangalla amesema kutokea kuuza karanga na BigG (bubble gum) mtaani mpaka kuwa Daktari, Mbunge na Kiongozi wa CCM Taifa na kufikia na ndoto ya kutegemea kugombea Urais ina maana moja tu kwamba sera za CCM zina tija kwa Taifa na wananchi wake na yeye ni mfano wa kwanza mkubwa wa kuaminiwa kwamba sera hizo zinajali usawa kwa wananchi kwani pamoja na kupitia yote aliyopitia bado anaweza kutuhubutu kugombea Urais wa Tanzania kwa kukubaliwa na kuruhusiwa kikatiba na chama chake CCM na kuruhusiwa kisheria na Sheria za Jamhuri ya Tanzania.






Posted By Unknown09:35

AL SHABAB WATANGAZA KIONGOZI MPYA BAADA YA KIFO CHA GODANE

Filled under:

Kundi la al-Shabab la nchini Somalia limemchagua Ahmed Umar (Ahmad Omar au Abu Ubaidah) kuwa mridhi wa Ahmed Abdi Godane (Abu Zubeyr) aliyeuawa katika mashambulizi yaliyoongozwa na Marekani siku ya Jumatatu kuamkia Jumanne ya wiki iliyopita.

Katika taarifa yake iliyonukuliwa na kituo cha habari cha Al Jazeera, kundi hilo limeapa kulipiza kisasi kwa mauaji ya mmoja wa waasisi wao likisema kuwa kifo cha mwanazuoni na kiongozi wao kinawalazimu kujitwika mabegani jukumu la malipo ambalo hawataliangusha wala kulisahau bila kujali muda wa kulikamilisha.

Kundi hilo limethibitisha kuuawa kwa Godane na viongozi wake wengine wawili.

Godane aliongoza al-Shabab tangu mwaka 2008 baada ya kifo cha mtangulizi wake, Aden Hashi Ayro ambaye naye aliuawa baada ya mashambulizi ya anga yaliyofanywa na Marekani huko kusini mwa mji wa Dhusamareeb.

Mashambulizi ya Jumatatu yalifanywa kwenye ngome ya al-Shabab huko Barawe yakimlenga Godane ambaye mwaka 2012 aliwekewa dau la dola za Kimarekani milioni $7 kama malipo kwa yeyote ambaye angewezesha na kufanikisha kukamatwa au kuuawa kwake.

Rais wa Somalia amekaririwa akiwataka wanamgambo wa al-Shabab kujisalimisha huku akiwapa siku 45 za msamaha kwa wapiganaji watakaotii wito huo.

Posted By Unknown09:20