Friday 28 February 2014

MAPACHA WALIOTENGANISHWA WAWASILI SALAMA KYELA

Filled under:

Kyela. Mamia ya wakazi wa Kijiji cha Kasumulu eneo la ‘Juakali’, wilayani Kyela Mkoa wa Mbeya, jana walimiminika nyumbani kwa mama wa watoto pacha, Grace Joel ili kushuhudia jinsi walivyotenganishwa baada ya kufanyiwa upasuaji nchini India hivi karibuni.

Watoto hao pacha, waliozaliwa wakiwa wameungana eneo la kiunoni, waliwasili na mama yao nyumbani kwao wilayani Kyela na kulakiwa na wanakijiji wengi.

Pacha hao, Elikana na Eliud wakiwa na baba yao, Rick Mwakyusa na mama yao, waliwasili kijijini kwa gari dogo.

Watoto na wazazi wao walifika kwenye nyumba anayoishi mzazi wa baba yao ambayo imejengwa kwa matofali ya kuchoma na kuezekwa kwa bati, lakini haina madirisha.

Miongoni mwa watu wa kwanza kushuhudia ugeni huo, alikuwa bibi wa watoto hao, Subilaga Kasekele ambaye ni mama wa Rick, akifuatana na mama mzazi wa Grace, Lide Mwakasala.


Kelele zililipuka kutoka kwa baadhi ya wanakijiji hao baada ya kupata taarifa za ujio huo na wengi waliwapokea kwa furaha kiasi cha kuwavuta hata watu kutoka vijiji vya jirani.

Mzazi wa watoto hao, Grace , akionekana mwenye furaha, alibubujikwa na machozi ya furaha na kuwashukuru wazazi wa pande zote mbili kwa maombi yao.

Akizungumzia hali yake, alimshukuru Mungu kwa kumfikisha salama Mbeya, lakini akasema ana wasiwasi na lishe ya watoto wake kwa kuwa hana uhakika wa kipato kwa kuwa hana kazi na mume wake ni dereva wa bodaboda.

“Nina wasiwasi na lishe kwa wanangu. Maisha yangu yenyewe ni ya ‘kubangaiza’, nimepanga nyumba kwa Sh.25,000 kwa mwezi, sasa baada ya hapo sijui...Nawashukuru Watanzania kwa misaada yao, lakini naomba wasiishie hapo,” alisema.

Alisema kuwa alichelewa kwenda Mbeya baada ya kuwasili Dar es Salaam kwani alikuwa akisubiri hati yake ya kusafiria pamoja na ripoti ya madaktari atakayoiwasilisha Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.

Watoto hao walirejea nchini Februari 20 mwaka huu, ikiwa ni siku moja kabla ya kutimiza mwaka.

Baba alonga 
Baba wa watoto hao, Mwakyusa alisema hana nyumba kijijini hapo bali amepanga na walihamia eneo hilo hivi karibuni wakitokea kijiji cha mbali zaidi.

Posted By Unknown23:14

MINIMUM WAGES IN TANZANIA WITH EFFECT FROM 2013-2016

Filled under:

 

Minimum Wages in Tanzania with effect from 01-07-2013 to 30-06-2016

Revision is expected.
Information last updated on this page: 06-02-2014
The minimum wage rates in the table are in TZS (TZ Shilling)
Sector Area Minimum Wage per Hour Minimum Wage per Day Minimum Wage per Week Minimum Wage per Fortnight Minimum Wage per Month
Health Services
677.00
5,077.33
30,463.90
60,927.76
132,000.00
Agricultural Services
512.85
3,846.50
23,078.70
46,157.40
100,000.00
Trade, Industries and Commercial Services Trade, Industry and Commerce
589.80
4,423.40
26,540.50
53,081.00
115,000.00
Financial Institutions
2,051.45
15,385.50
92,314.80
184,629.60
400,000.00
Communication Services Telecommunication Services
2,051.45
15,385.80
92,314.80
184,629.60
400,000.00
Communication services Broadcasting and Mass Media, Postal and Courier Services
769.30
5,769.70
34,618.05
69,236.10
150,000.00
Mining Mining and prospecting licenses
2,051.45
15,385.80
92,314.40
184,629.60
400,000.00
Primary Mining Licences
1,025.80
7,692.90
46,157.40
91,314.80
200,000.00
Dealers licenses
2,367.10
11,539.35
69,236.10
138,472.20
300,000.00
Brokers licenses
1,025.80
7,692.90
46,157.40
200,000.00
Private schools services (Nursery, Primary and Secondary schools)
718.00
5,385.02
32,310.15
64,620.35
140,000.00
Domestic and Hospital Services Domestic Workers employed by Diplomats and Potential businessmen
769.30
5,769.70
34,618.05
69,236.10
150,000.00
Domestic Workers employed by entitled officers
666.70
5,000.40
30,002.30
60,004.60
130,000.00
Domestic Workers other than those employed by diplomats and potential businessmen and entitled officers who are not residing in the household of the employer
410.30
3,077.15
18,463.00
36,925.90
80,000.00
Other domestic workers
40,000.00
Potential and Tourists hotel
1,282.15
9,616.10
57,696.75
115,393.50
250,000.00
Medium Hotels
769.30
5,769.65
34,618.05
69,136.10
150,000.00
Restaurants, Guest Houses and Bars
666.70
5,000.40
30,002.30
115,393.50
130,000.00
Private Security Services International or potential security Companies
769.30
5,769.65
34,618.05
69,136.10
150,000.00
Small companies
512.85
3,846.50
23,078.70
46,157.40
100,000.00
Energy Services International Companies
2,051.45
15,385.80
92,314.80
184,629.60
400,000.00
Small companies
769.30
5,769.65
34,618.05
69,136.10
150,000.00
Transport Services Aviation Services
1,795.05
13,462.55
80,775.45
161,550.90
300,000.00
Clearing & Forwarding
1,538.78
11,539.35
69,136.10
138,472.20
300,000.00
Inland Transport
1,025.80
1,025.80
46,157.40
92,314.80
200,000.00
Construction Services Contractor Class I
1,666.80
12,500.95
75,005.75
150,011.50
325,000.00
Contractors Class II-IV
1,435.05
10,770.05
64,620.35
129,240.70
280,000.00
Contractors Class V-VII
1,282.15
9,616.10
5,769.75
115,393.50
250,000.00
Fishing and Marine Services
1,025.80
7,692.90
46,157.40
92,314.80
200,000.00
Other sectors not mentioned above
512.85
38,446.45
23,078.70
46,157.40
100,000.00

Posted By Unknown22:24

FAHAMU NJIA SAHIHI ZA KUCHAGUA MTU WA KUISHI NAYE

Filled under:



MARA nyingi vijana hupata taabu sana katika suala la kuchagua mchumba. Vijana wa kiume ndio hasa hupata wakati mgumu zaidi kwani jamii imewapa wajibu wa kuanzisha mazungumzo 

yahusianayo na mapenzi. Hata hivyo, vijana wa kike nao wanao wajibu wa kuchagua ili kuhakikisha kuwa hawaanguki mikononi mwa mabazazi wa kuwalaghai na kuwatumia kwa raha za miili yao kisha kuwaacha kwenye mataa.

Ni jambo la kawaida kwa vijana walio wengi, wawe wa kike au wa kiume, kuangalia sura na mwonekano wa mtu. Lakini unapotafuta mchum ba kwa malengo ya kuishi naye maisha yako yote kama mume na mke haipendezi kuangalia tu mwonekano, maana Waswahili husema si kila king’aacho ni almasi. Kwa sababu hiyo, hapa yatabainishwa mambo muhimu ya kuangalia na kuzingatia katika suala hili.

1. UADILIFU
Pamoja na sifa zote za uzuri zinazoweza kubainishwa na kufanywa kuwa vigezo vya uzuri wa mwanamke na mwanaume na hata zikatumiwa kumpata Miss au Mr Tanzania, sifa kuu impasayo mtu anayefaa kuwa mchumba kuwa nayo ni sifa ya uadilifu.

Mtu anapokuwa na uadilifu (pengine uaminifu), maana yake ni kwamba tabia ya mtu huyu anayoionesha nje ndiyo tabia yake halisi na anapofanya jambo jema analifanya kwa roho yake na si kwa unafiki.

Mtu anapokuwa mwadilifu ataheshimu maadili na kufanya wema, hata pale inapokuwa rahisi kwa wengine kukengeuka na kufuata njia za mkato ambazo mara nyingi si za halali.

Mtu mwadilifu pia huwa na sifa za ukweli na kujitolea kuwasaidia watu wengine bila kujali faida – haya yote ni mambo muhimu ambayo mtu mwenye kuwa nayo huwa na msingi wa ujenzi wa uhusiano imara na wa kudumu.

Watu wanaoweza kujivunia furaha ya kweli katika maisha yao ya ndoa, ni watu ambao wamekutana wote wakiwa na sifa ya uadilifu ambayo hujumuisha mambo mengi.

Zipo ndoa nyingi zenye furaha ya bandia. Furaha hii mara nyingi hutokana na ridhiko la kimwili alipatalo mtu kutokana na kukidhiwa kwa mahitaji yake ya kimwili yanayohusiana na haki za msingi za binadamu – yaani chakula, mavazi na malazi. Lakini furaha ya kweli ya maisha ya ndoa, watu hawaipati isipokuwa katika uhusiano ambao wenza wamethibitishana kuwa waadilifu.

2. HEKIMA
Mtu mwenye uadilifu wa kweli, mbali na kuwa mwema kwa mwenzake, pia huhakikisha anakabiliana kwa busara na hekima na matatizo yote yanayoweza kusababisha kuyumba kwa uhusiano, hususan yale yaliyo nje ya uwezo wake.

Uzoefu unaonesha kuwa wapenzi, hususan wanandoa walio katika uhusiano wa muda mrefu wanaoendelea kufurahia unyumba wao si wale ambao walipendana kwa mvuto na wala hawana mambo mengi ya asili yanayowaunganisha kuliko wale wanaotengana. 

Lakini la muhimu ni kwamba watu hawa huwa wamejifunza jinsi ya kukabiliana kwa hekima na matatizo yanayojitokeza, hususan yale yanayotokana na tofauti zao kimtazamo.

Ukiachilia mbali sifa ya uadilifu, watu hawa huwa wamejifunza kukabiliana na matatizo kuhusiana na uzazi na ulezi wa watoto, uhusiano na ndugu, jamaa na marafiki, suala la ngono, fedha na maisha ya unyumba kwa ujumla.

Habari njema ni kwamba uadilifu na hekima ni mambo ambayo mtu yeyote anaweza kujifunza na kisha kufanyia kazi. Ndiyo maana wanandoa hufundishwa kabla ya ndoa na hata wanapokuwa tayari wameoana huendelea kuhudhuria semina za kidini na kijamii kwa ajili ya kujiimarisha.

Kwa hiyo, kama mume/mke wako mtarajiwa anaonekana kuwa na utayari wa kujifunza kuhusiana na jinsi ya kuishi na mtu wa jinsia nyingine, ana nafasi kubwa ya kuwa mke/mume mzuri baadaye.

3. UPOLE
Mfalme Suleiman katika mojawapo ya semi zake za hekima alisema mwanamke mpumbavu huibomoa nyumba yake kwa mikono yake. Yamkini ndivyo ilivyo pia kwa mwanaume mpumbavu, maana upumbavu haujengi.

Siku zote kitu kinachovunja uhusiano wa kindoa si makombora ya nyuklia, bali ni ulimi. Kwa kadri mtu anavyoutumia ulimi wake anaweza kuijenga au kuibomoa nyumba yake.

Katika kumwangalia mtu ambaye unaweza kujenga naye nyumba ya kudumu, ni vema kumchunguza na kuhakikisha kuwa si mtu mwenye kupenda kurefusha maneno, maana hakika huyu atasababisha ugomvi mara kwa mara na uhusiano hautadumu.

Wapo watu ambao ndoa zao zina sifa ya ugomvi na karibu kila mtu anafahamu na hata wamekuwa kero kwa ndugu, jamaa na majirani zao, mara kwa mara wakiwaamsha watu usiku wa manane wakitafuta suluhu.

Mara nyingi wanaume ndio huanzisha ugomvi, lakini ugomvi huwa na nguvu zaidi kama mwanamke ni msemaji. Dawa ya kuzuia ugomvi usiokuwa na mpango ni kupunguza maneno na kuepuka kutafuta ushindi katika ubishi. Lakini kinga ya tatizo hili ni kuepuka kujiingiza katika uhusiano na mtu ambaye umejihakikishia kuwa si mwingi wa maneno.

Bahati nzuri, jamii huwatambua wanawake/wanaume ambao wanaweza kuwa wake/waume bora baadaye kwa hiyo ni wajibu wa mtafutaji kuhakikisha kuwa anafanya uchunguzi wa kina kabla ya kujitosa kwa mtu ambaye baadaye atamtaabisha.

Mwanandoa aliyeifahamu vema dhana ya ndoa – kwamba ni maisha ya kuvumiliana na kuchukuliana, hufahamu ni wakati gani wa kusema na wakati gani wa kukaa kimya. Mtu huyu pia hufahamu njia nzuri na salama ya kujiondoa kwenye tatizo anapoona mwenzake anaelekea kubaya, ili hatimaye uhusiano wao uendelee kuwa salama japo wao wanaweza kuwa wamekwaruzana.
Mtu huyu mwenye upole hujiweka katika mkao wa upatanishi na huhakikisha kuwa kila mjadala mkali unapita na kumalizika salama. Ni wazi kuwa katika kutafuta, kama hukukurupuka, utamwona mtu mwenye hulka hii – upole.
4. MVUTO
Hisia za mvuto wa kimapenzi ni muhimu katika kujenga uhusiano. Mtu mmoja akauliza, ni yupi bora – yule anayenivutia sana au yule anayenipenda sana? Maisha ni ya ajabu sana. Huwa inatokea kuwa mtu unayevutiwa naye sana yeye havutiwi nawe, bali anavutiwa na mwingine ambaye naye hana mpango naye!

Haya ndiyo maisha. Uzoefu unaonesha kuwa asilimia kubwa ya watu walio katika ndoa hawajawaoa/kuolewa na watu waliokuwa wakiwapenda sana enzi za ujana wao, au wale waliotimiza ndoto za ujana wao. Bahati njema miongoni mwa wanandoa hawa wapo wale wenye ndoa imara sana.

Mvuto wa kimapenzi ni muhimu sana, lakini watu husema maji yakisema usininywe yajibu kuwa wewe pia huna kiu nayo. Japo inaweza kuonekana kama ni aina ya ‘sizitaki mbichi hizi’ lakini si vema kujisumbua na mtu asiyekupenda.

Badala ya kujihangaisha na mtu asiyekupenda, kaa chini na umsubiri anayekupenda hata kama huhisi kuvutiwa naye sana. Baadaye utamzoea na maisha yatakuwa mazuri, kisha utajiuliza baadaye yule aliyekuringia alikuwa na nini cha ziada?

Lakini iwapo mambo mengine yote yatakwenda sawa, ni vema na muhimu kabisa kuhakikisha kuwa mtu unayepanga kuwa naye maisha yako yote ni mtu anayekuvutia kimwili na kiakili, maana vinginevyo unaweza kupata sababu ya kukidhi kiu yako nje – jambo ambalo si maadili mema katika ndoa na maisha.

NI MUHIMU KUWA MAKINI
Katika nyakati za ujana, watu wengi hubabaishwa kwa mengi. Vijana wa kiume hubabaishwa na sura, maumbile na pengine rangi na kusahau mambo muhimu yaundayo orodha ya sifa za mke mwema.
Kwa upande wao, vijana wa kile pia waweza kubabaishwa na pesa, maumbile, sura, utanashati, umaarufu au kuchoshwa na shinikizo la umri, hivyo kujikuta wakijitumbukiza kwa wanaume wasio na sifa za waume wazuri.
Lakini tukirejea kwenye msemo wa zamani kuwa uzuri si hoja bora tabia, ni wazi kuwa tutafikia mahali tutajenga mahusiano imara na yasiyotikiswa na sunami zozote za kimaisha. Ilimradi tu uhakikishe kuwa mtu mwenyewe anakupa mvuto kimapenzi, maana vinginevyo kutakuwa hakuna maana.

Posted By Unknown11:55

DOGO ASLAY ATIRIRIKA KUHUSU MATOKEO YAKE YA KIDATO CHA NNE

Filled under:

Dogo Aslay

 BAADA ya kupata matokeo mabaya kidato cha nne, kinda wa muziki wa kizazi kipya nchini, Asilahi Isihaka ‘Dogo Aslay’ amesema anatarajia kusoma chuo cha muziki ili kukuza kipaji chake.

Akizungumzia matokeo hayo, Aslay alisema hajasikitika sana kupata matokeo hayo na wala hajakata tamaa ya kuendelea kusoma, kwani anataka kusomea muziki kwa lengo la kuongeza ‘mautundu’ katika kazi zake.

“Nimepata 4 ya pointi 32, kwa sababu nilikuwa nachanganya muziki na masomo, hivyo sijayachukia sana matokeo hayo na kwa kuwa muziki ndio kitu ninachokipenda, nataka kusoma chuo cha muziki na si kupoteza muda kuanza ‘kurisiti’, bado sijajua nitakwenda chuo gani kwa ajili ya masomo hayo,” alisema.

“Wengi wamekuwa wakinisema kwamba napoteza muda mwingi kwa kufanya muziki na kusahau masomo, ndiyo maana nafeli, mwisho wa siku ukweli unabaki pale pale napenda muziki ndiyo maana nafanya vizuri na ndiyo maana nataka nikaongeze elimu katika muziki wangu,” alisema Aslay.

Dogo Aslay ni kati ya wasanii wenye umri mdogo ambao wanafanya vizuri katika muziki huo, huku akitambulishwa na ngoma yake ambayo ilibamba vilivyo ‘Naenda Kusema kwa Mama’.

Posted By Unknown11:12

NYALANDU AFIKISHA ORODHA YA WATU 320 WANAOJIHUSISHA NA UJANGILI

Filled under:


PAMOJA na serikali kutotaja majina ya watu 40 ambao Rais Jakaya Kikwete alisema ndio mtandao wa ujangili nchini, akiwemo tajiri maarufu mkoani Arusha, Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, amesisitiza kuwa orodha hiyo si ya kutengeneza na kwamba itawekwa hadharani muda wowote. 

Alisema kuwa wanayo majina zaidi ya 320 ya watu wanaojihusisha na ujangili na kuonya wahusika kuachana na biashara hiyo huku akitamba kuwa serikali ina mkono mrefu.

Waziri Nyalandu alitoa msimamo huo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari wizarani kwake kueleza juhudi za serikali katika kukabiliana na ujangili nchini.

Posted By Unknown11:06

KURA YA WAZI YA RASIMU YA KATIBA ITALETA UHASAMA

Filled under:



HATULITAKI Kundi dogo la watu wenye nguvu ya Fedha na matakwa yao binafsi miongoni mwa wajumbe wa Bunge la katiba, wanaopinga kura ya siri wakitaka iwepo kura ya wazi bungeni humo, ambayo tuna imani kubwa kwa vyovyote italeta Uhasama.
Tumekuwa tukishuhudia Viongozi wa Serikali na Wabunge wao, wakijifungia kwenye kumbi kuweka misimamo na maagizo ya vyama vyao! Ningetoa rai tusingependa kuona kura ya wazi yenye majanga, visa, vifo na umwagaji damu, inaidhinishwa na wabunge wa rasimu hii.

Ikumbukwe; Tumechoshwa kuona damu zisizo na hatia zinamwagika kila mara kwa sababu ya mashinikizo ya wana siasa wachache wenye uroho na ubinafsi wa madaraka, ambao kila siku wanapigia upatu waendelee kuwa na nyadhifu na vyeo vya kutoa Kafara.

Kutoka na uzoefu tuliouona nyakati za vikao vya Bunge la Muungano, ambapo hupiga kura za ndiyo na hapana ambazo kwa sehemu kubwa huwa hazina usahihi kutokana na kuamuliwa kwa udhaifu wa wingi wa sauti za watu, historia ya Bunge hili Maalum la Katiba si la ulegelege huo.
Tuna ushahidi; Iwapo utaratibu wa kura ya wazi utatumika kwenye maamuzi ya Bunge Maalum, utaminya haki na kuwapa haki watu wenye uwezo wa kushinikiza watu wapige kura kwa uoga na mashinikizo ya fedha au vitisho.
Hatuipendi kura ya wazi kwa sababu, inaweza kumpa fursa Mwenyekiti wa Bunge hilo asiyekuwa makini, kuunyima au kuupatia upande wenye sauti kubwa ya fedha kujibu hata kama ni wachache, na ukapate kura ambazo hata kama zilikuwa za watu wengi lakini hawana sauti ya hela.
Kura ya wazi inamkaba mpigaji kutokuwa na uhuru, na kwamba anaweza kubadili mawazo na makusudi aliyokuwa nayo kutokana na kuona anayehusika na kitu wanachokipigia kura, hivyo kwa Fadhira, Huruma au Woga wa kununiana na kueleweka vibaya, akalazimika kupigia upande wake.
Kura ya wazi ina mwanya mkubwa wa kupenyeza Rushwa, ambapo ikitokea wakati wa kupiga kwa wazi kwa maana ya kunyosha vidole, kusimama nyuma ya mtu au kujibu ndiyo au hapana kwa kuitwa majina; ni dhahiri kutakuwa na uhasama na visasi vyenye maafa baadaye, kama mtu ataacha kumchagua

Rai hii inafuatia kuanza kujitokeza vikao hivyo (Part Cocas) kwa vyama katika kumbi zilizozoeleka wakati wa Bunge la Kawaida la Muungano, ambapo kwa Bunge hili Maalum, tunahoji, wajumbe wa Taasisi wasiokuwa na kumbi watakutana wapi? Kwa nini Wabunge hawajui kuwa hili si Bunge la vikao vya Muungano?

Tulikuwa tunatarajia kama kunakuwa na vikao vya kujadili mustakabali wa Rasimu namna hiyo, basi wabunge wote zaidi ya 600 wangekaa pamoja na kujadiliana mapungufu na nyongeza nzuri za maandiko ya rasimu hiyo, lakini vyama vinapojigawa kwa itikadi zake haituingii akilini.

Migawanyo hiyo kama inafanywa na Serikali au Viongozi wake, ni kinyume cha Sheria ya Rasimu hiyo, maana jopo hilo lililoteuliwa, linatakiwa liwe pamoja kama timu kujadili mustakabali wa rasimu hiyo bila kuwa vipande vipande vya mijadala vinavyofanywa hivi sasa kwa kujifungia kwenye kumbi au vyumba.

Kama mipaka na migawanyo hiyo itaendelea, ni dhahiri mwisho wa yote tutakuwa na Katiba ya mashinikizo iliyojaa ubabaishaji ambayo itakuwa Janga na watanzania wategemee kulia kwa mateso yatakayotokana na Katiba Ubabishaji kwa mika Mingi, huku Kodi ya wananchi ikiwa imepotea.

Posted By Unknown10:52

Thursday 27 February 2014

SLAA:KUMPITISHA CHENGE NI MAJANGA

Filled under:



Wakati  Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, akitajwa kuwa miongoni mwa wajumbe wa Bunge la Katiba watakaowania uenyekiti wa bunge hilo, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa, amesema mbunge huyo hafai kwa kuwa uadilifu wake una walakini.

Dk. Slaa amewapa angalizo wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wakiwamo wa kutoka chama chake kwamba watajuta kwa miaka mingi iwapo watamchagua Chenge kuwa Mwenyekiti wa bunge hilo.

Alisema uadilifu wa Chenge unatia shaka kwa kuwa anakabiliwa na tuhuma za kuhusika katika kashfa ya ununuzi wa rada ya kijeshi ambayo serikali iliinunua kwa fedha nyingi kuliko thamani yake kutoka Uingereza wakati akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali mapema miaka ya 2000.

“Katiba hii, sisi (Chadema) ndiyo waasisi wake katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 na baada ya hapo ndipo wenzetu (CCM) walipoidandia na kutangaza nia ya kusaka katiba mpya. Yote sawa, lakini nitashangaa sana na wala sitegemei itokee Andrew Chenge akachaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Bunge hilo...Na wabunge wangu

wanafahamu machungu yatakayojitokeza iwapo watamuunga mkono Chenge,” alisema Dk. Slaa wakati akimnadi mgombea ubunge wa Chadema katika Jimbo la Kalenga, Grace Tendega, katika mkutano wa hadhara wa kampeni.

Dk. Slaa alisema licha ya kukabiliwa na tuhuma hizo, Chenge hadi sasa hajasafishwa.

Akizungumza katika mkutano huo uliofanyika katika kijiji cha Igula kata ya Luhota, Dk. Slaa alisisitiza kuwa wajumbe wa Bunge la Katiba hawapaswi kufanya makosa katika uchaguzi huo kama kweli wana nia ya dhati ya kupata katiba mpya itakayokuwa imebeba mawazo ya Watanzania wote na si ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Wakati Dk. Slaa akitoa angalizo hilo, Mjumbe wa Bunge hilo na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ametaja sifa za mgombea wa nafasi ya mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba anayepaswa kuungwa mkono kuwa ni yule atakayelinda heshima ya mawazo ya wananchi kuhusu katiba mpya pamoja na hadhi na heshima ya Bunge hilo.

 Profesa Lipumba aliliambia NIPASHE jana kuwa sifa hiyo ya mgombea wa nafasi hiyo ndiyo hasa msimamo wa Umoja wa Katiba ya Wananchi, ambao yeye na chama chake ni wajumbe wake.

 Profesa Lipumba alisema baada ya umoja huo kuundwa, wanachokisubiri hivi sasa ni wajumbe wa Bunge hilo kupitisha Rasimu ya Kanuni za Bunge hilo.
“Sisi tutamuunga mkono (mgombea) yule mwenye uwezo wa kutoa heshima kwa mawazo ya wananchi na hadhi ya Bunge bila kujali anatoka chama gani,” alisema Profesa Lipumba.

MWENYEKITI KUCHAGULIWA JUMAPILI
Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa kudumu wa Bunge Maalum la Katiba, anatarajiwa kupatikana Jumapili wiki hii.

Habari zilizopatikana mjini hapa jana zilieleza kuwa, zoezi la uchukuaji wa fomu za kuomba kuwania nafasi hiyo litafanyika Jumamosi.

Kwa mujibu wa habari hizo leo ambayo awali ilipangwa kwa ajili ya kuwapa wajumbe wa bunge hilo semina kuhusu rasimu ya kanuni za bunge maalum pekee, sasa itatumika pia kwa wajumbe hao sambamba na kujadili rasimu hiyo ya kanuni.

Habari hizo zinasema kuwa semina hiyo itaendelea hadi kesho na kwamba Ijumaa bunge litapitisha azimio la kuipitisha rasimu ya kanuni hizo.

Habari hizo zinasema kuwa baada ya uchaguzi wa Mwenyekiti, litafuatia zoezi la Rais kumuapisha Katibu wa Bunge la Katiba na Naibu Katibu wa Bunge hilo wiki ijayo.Katibu wa Bunge atamwapisha Mwenyekiti, ambaye naye atawaapisha wajumbe.

Hata hivyo, Katibu wa Bunge Maalum la katiba, Dk. Thomas kashillilah, hakupatikana kutoa ufafanuzi.

Katika hatua nyingine, wajumbe wa CCM jana walikuwa na kikao kilichotarajiwa kuanza saa 1:00 jioni pamoja na mambo mengine, kuweka msimamo kuhusiana na mgombea wake wa uenyekiti.

Hadi sasa wanaotajwa kugombea nafasi hiyo mbali na Chenge ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta.

Posted By Unknown05:38

ITS MASTER'S SCHOLARSHIP FOR UK,INTERNATIONAL STUDENT IN UK 2014/15

Filled under:



The Institute for Transport Studies (ITS) at University of Leeds is offering masters scholarships for UK, EU or international students. Applicants must first hold an offer (conditional or unconditional) of an academic place on an ITS Masters programme for the academic year commencing September 2014. The scholarships provide a 50% tuition fee waiver for the 2014-15 academic year. Application should be submitted till 12th June 2014 (international applicants) and by 7th July 2014 (UK/EU applicants).
Study Subject (s): Scholarship applications can be made for any of the five programmes: MA Transport Economics, MSc Sustainability (Transport), MSc Transport Planning, MSc Transport Planning and the Environment and MSc (Eng) Transport Planning and Engineering at ITS. Course Level: Scholarships are available for pursuing master degree at ITS, University of Leeds. Scholarship Provider: The Institute for Transport Studies (ITS), University of Leeds Scholarship can be taken at: UK
Eligibility: Applicants must first hold an offer (conditional or unconditional) of an academic place on an ITS Masters programme for the academic year commencing September 2014.
Scholarship Open for International Students: UK, EU or international students can apply for these masters scholarships.
Scholarship Description: The Institute for Transport Studies (ITS), University of Leeds, is offering a number of fees scholarships, each worth up to £7750, to provide development opportunities to students of outstanding ability, achievement and potential. The scholarships will fund 50% of the tuition fees for UK, EU or international students to undertake a full-time Masters degree programme at ITS. The scholarships form part of the ITS mission to advance the understanding of global transport, via the development of future transport professionals. Scholarship applications will be assessed on a competitive basis, and it is anticipated that up to five awards will be made.
Number of award(s): It is anticipated that up to five awards will be made.
Duration of award(s): Not Known
What does it cover? The scholarships provide a 50% tuition fee waiver for the 2014-15 academic years. (equivalent to the value of £7750 for international students or £2750 for UK/EU students).
Selection Criteria: Scholarship applications will be assessed on a competitive basis.
Notification: Not Known
How to Apply: Applicants should submit the ITS scholarship form, including a statement of 500 words on how a Masters degree would enable them to make a difference to transportation (e.g. in their country, region or area) and specifically to tackle a significant problem or issue.
Scholarship Application Deadline: Scholarship applications should be submitted to ITS no later than 12th June 2014 for international applicants and by 7th July 2014 for UK/EU applicants.

Posted By Unknown05:17

WIT INTERNATIONAL STUDENT SCHOLARSHIPS IN IRELAND,2015

Filled under:



Waterford Institute of Technology is offering international scholarships for pursuing undergraduate or a Higher Diploma programme and taught Masters programmes. Scholarship will provide a 25% reduction in tuition fees for each year of an undergraduate or a Higher Diploma programme and a reduction of €3150 for all taught Masters programmes. Application should be submitted till 31st May 2014 for September 2014 intake.
Study Subject (s): Scholarships are awarded to learn any of the courses available at Waterford Institute of Technology. Course Level: Scholarships are available for pursuing undergraduate or a Higher Diploma programme and taught Masters programmes at Waterford Institute of Technology. Scholarship Provider: Waterford Institute of Technology Scholarship can be taken at: Ireland
Eligibility:
-The scholarships are open to all self-funding Non-EU students
-Minimum IELTS score of 6.5 or equivalent

Scholarship Open for International Students: International (Non-EU) students can apply for the scholarships.
Scholarship Description: WIT is pleased to offer International student scholarships in all disciplines at WIT for undergraduate and postgraduate students commencing their studies in September 2014. Diversity of students in terms of country of origin is one of the pillars on which international education in any institution is founded. In order to encourage high calibre applicants to study at our Institute, they offer a number of scholarships to Non-EU citizens on an annual basis.

Number of award(s): A number of scholarships are available.
Duration of award(s): International Student Scholarships will be awarded for the duration of the programme. Award in subsequent years of study is subject to the achievement of 60% overall average mark.
What does it cover? The International Student Scholarship will provide for a 25% reduction in tuition fees for each year of an undergraduate or a Higher Diploma programme. (NB for entry into all years of Bachelor programmes except final year). Award in subsequent years of study is subject to the achievement of 60% overall average mark (Undergraduate and Higher Diploma students). The International Student Scholarship will provide for a reduction of €3150 for all taught Masters programmes (Postgraduate students).
Selection Criteria: Not Known
Notification: Successful applicants will be notified by mid-June 2014.
How to Apply: Applicants should apply by post.
Scholarship Application Deadline: The application deadline is 31st May 2014.
Further Official Scholarship Information and Application

Posted By Unknown05:10

DENMARK SCHOLARSHIP,2014

Filled under:


Do you aspire to take up your study in Denmark? Luckily, there are a wide range of scholarships in Denmark that you can look out in 2014. Denmark has emerged as a leading destination for overseas students anticipating for an international education. All the available scholarships in Denmark assist both Danish and international students to pursue their studies in Denmark as well as in any part of the world by offering excellent financial support. Listed financial aids and awards are provided for diverse programs like graduate, postgraduate, PhD and research degree levels in manifold academic disciplines. Figure out here different types of scholarship opportunities and pay the costs of your education. To get started on sponsoring your appealing future, click on the following details to learn about scholarships in Denmark that are feasible and how to apply:
Upper Midwest Rebild Scholarship Corporation in Denmark
The Upper Midwest Rebild Scholarship Corporation supports U.S. university students who study abroad in Denmark. This award, up to $3,000, supports a student of Danish background or one who has demonstrated a strong interest and commitment to Denmark. The application deadlines are 1st March 2014, April 1, 2014 and October 1, 2014.

Faculty of Science PhD Positions in Denmark
The Department of Geosciences and Natural Resource Management (IGN) offers four fully financed PhD positions to highly skilled candidates commencing May 1, 2014 or as soon as possible thereafter. The grants only include salary for the PhD student and a small annual supplement covering educational costs. The application must be received no later than April 1, 2014.

AIAS-COFUND (Marie Curie) Fellowships in Denmark
Aarhus Institute of Advanced Studies (AIAS) is funding up to 25 AIAS-COFUND fellowships that are available for talented researchers in the first round of applications. The target group of the programme is talented researchers with at least two years of fulltime experience after completing their PhD. Applicants can choose their research topic freely within all academic areas. The deadline for applications is 21st March 2014.

Faculty of Sciences PhD Fellowships in Denmark
Fellowships are available for pursuing PhD degree at University of Copenhagen in Denmark. The positions are available for a 3-year period for applicants holding a relevant master´s degree. Applicant must Fluent in spoken and written English. 3 PhD fellowships are offered. The application deadline is March 19, 2014.

Danish Long-Term Scholarships in Denmark
Scholarships in Denmark are only available to master’s and PhD-level students. However, bachelor’s degree students wishing to study Danish language and literature can also apply if they have studied the Danish language for two years. Applications should be submitted by 1st March, 2014.

Danish Summer Language Scholarships in Denmark
The summer language course scholarships in Denmark are available for students enrolled in full-time bachelor, master’s and PhD degree. These scholarships are available for the students of selected institutions. Applicants can apply for the scholarship under the Cultural Agreements programme to attend a Danish Summer Language Course.  The deadline for applications for Group 1, 2 or 3 for Danish summer language courses in 2014 is March 1, 2014.

Scholarships in Denmark for Non-EU Students
University College Lillebaelt is offering scholarships in Denmark for the non EU students. The scholarships will cover tuition fees and contribute to living expenses while studying at UCL. Applicants must be enrolled in a full degree higher education programme in your home country related to either nursing, social education or teacher education. Applications will be available in February.

Erasmus Mundus Joint Doctorate Programme
The programme will be opened for the students who will fully integrated three-year PhD programme. Selected doctoral candidates should expect to start their doctoral studies around 1 September every year. Each of the three categories is given a score from 1 (poor) to 5 (excellent); eligible applicants must not score 3 or lower in any category. The applications will be available in June 2014.

All the Best!!
Regards
Sneha Asanani

Scholarship Tags: , , , , , , , , ,

Read more: Denmark Scholarships, 2014-2015 : Scholarship

Posted By Unknown05:03

Wednesday 26 February 2014

UGANDA YAHOFIA KUNYIMWA MISAADA KISA!!!!!

Filled under:


Waziri wa mambo ya nje nchini Uganda, Sam Kutesa amesema ana wasiwasi kuwa Marekani huenda ikasitisha msaada wake kwa taifa hilo baada ya Rais Yoweri Museveni kuidhinisha sheria dhidi ya ushoga nchini humo.
 A
Bwana Kutesa amesema kuwa watu sharti wawe na maadili na kukubali msaada.
Balozi wa Marekani nchini Uganda Scott DeLisi, awali aliitaka serikali ya Uganda, kubatilisha sheria hiyo.

Alisema alihitaji kufafanuliwa zaidi sheria hiyo, kabla ya Marekani kujua ikiwa itaendelea na mipango yake ya misaada kwa nchi hiyo hasa miradi ya kupambana dhidi ya HIV na Ukimwi..
Sheria hiyo mpya, inatoa adhabu kali kwa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja na kupiga marufuku kile inachosema kusambaza vitendo vya ushoga.

Posted By Unknown10:17

SLAA:ANAYETAKA KUONDOKA CHADEMA RUKSA

Filled under:

 
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amesema kuwa mbunge au diwani anayetaka kuondoka CHADEMA milango iko wazi, kwa sababu hawawezi kumvumilia kiongozi msaliti wa chama. Dk. Slaa alitoa msimamo huo jana wakati akimnadi mgombea ubunge wa CHADEMA jimboni Kalenga, Grace Tendega, katika mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa mnadani, Kijiji cha Kidamali, Kata ya Nzihi huku akisisitiza kuwa wameridhia kujiuzulu kwa madiwani wao wawili mkoani Shinyanga. Alisema kujiuzulu kwao ni mpango maalumu uliotengenezwa na wapinzani wao kisiasa kwa lengo la kuwadhoofisha na kuwavuruga.

Posted By Unknown09:30

Tuesday 25 February 2014

ANASWA MUHIMBILI AKIDAIWA KUFANYA MATIBABU KINYEMELA

Filled under:



Maofisa Usalama wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), wamemkamata mtu anayedaiwa kutoa huduma kwa wagonjwa kinyume cha utaratiba na kwamba, amekuwa akiwatapeli wagonjwa wanaokwenda kupata matibabu.
 
Akizungumza ofisini kwake jana, Ofisa Uhusiano wa MNH, Aminieli Eligaesha alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Mustafa Kitano na kwamba, amekuwa akitumia majina ya Dk Nyirabu na Koba, alikamatwa wakati akimsaidia mgonjwa mmoja.
Eligeisha alisema Februari 22 mwaka huu walipata taarifa kutoka kwa Hussein Haji kuwa, kuna daktari anaitwa Koba alitaka kumtapeli Sh200,000 ili amtafutie kazi ya udereva kwenye tawi la MNH lililopo Kahama Shinyanga.
Inadaiwa Haji alipofika Muhimbili alimpigia simu daktari huyo, lakini aliambiwa kuwa wasingeweza kuonana kwa sababu alikuwa ana kikao na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, badala yake alimtaka akutane na Dk Said Kiliwanga.
“Alimwambia kazi hiyo utakuwa analipwa Sh570,000 na posho kila siku Sh90,000, pia alimwambia amtumie namba yake ya leseni,” alisema Eligaeshi.
Akisimulia jinsi alivyonusurika kutapeliwa, Haji alidai Dk Kiliwanga (ambaye hajakamatwa) alimtaka atume fedha kwenye M-Pesa ili waonane, kitendo alichokataa na kwenda kutoa taarifa kwa walinzi wa hospitali hiyo.

Namna alivyonaswa
Eligaeshi alidai maofisa usalama wa hospitali hiyo walipata taarifa za kuwapo kwa daktari aliyeonekana akiwahudumia wagonjwa na kwenda kumkamata.
Baada ya kutiwa mbaroni, inadaiwa alipekuliwa na kukutwa na kadi tatu za kliniki za wagonjwa wa Muhimbili, kitambulisho cha Peter Daniel mfanyakazi wa hoteli moja Dar es Salaam, vipimo vya kupimia ujauzito, namba nyingi za madaktari wa Muhimbili kwenye simu yake ya mkononi na Sh167,000. Wakati akiwa chini ya ulinzi, mmoja wa wagonjwa wake, aliyefahamika kwa jina la Hassan Madika alimpigia simu na kutakiwa kwenda sehemu aliyokuwa akihojiwa. Mtuhumiwa alikiri kupigiwa simu na Madika.

Kitano ajitetea
Kitano alisema kuwa alifika hospitalini hapo baada ya Madika kumweleza kuwa alikuwa amefanyiwa operesheni wiki iliyopita na kwamba, hawezi kusimama muda mrefu hivyo alikuwa akihitaji msaada wa mtu wa kumpelekea faili sehemu husika.
Haji alipoulizwa na waandishi wa habari, iwapo anamfahamu Kitano alisema alikiri kutomfahamu na kwamba, hajawahi kumwona.

Alisema alifika hospitalini hapo kumsaidi Madika na kwamba, tuhuma hizo zinalenga kumchafulia jina hazina ukweli.
Hata hivyo, Kitano alisema yeye siyo tapeli daktari na ameshafanya kazi hospitali mbalimbali za Serikali.

Posted By Unknown19:54