Thursday 30 October 2014

AJIRA: MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO TANZANIA AUTOMOTIVE TECHNOLOGY CENTRE

Filled under:

MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO OFFICE ASSISTANT - NYUMBU
WASAILIWA WALIOFANIKIWA KUENDELEA NA USAILI WA MAHOJIANO, MAHALI: NYUMBU - KIBAHA TAREHE 30-10-2014 SAA MOJA KAMILI ASUBUHI.
KADA: OFFICE ASSISTANT

EXAMINATION NUMBES    SCORE    REMARKS
PSRS NYUMBU OA 0022    55    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0042    55    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0024    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0028    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0036    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0041    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0004    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0034    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0039    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0050    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0014    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0017    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0031    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0005    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0006    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0047    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0001    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0002    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0010    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0019    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0023    40    NOT SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0027    40    NOT SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0048    40    NOT SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0012    35    NOT SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0052    35    NOT SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0037    35    NOT SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0045    35    NOT SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0009    5    NOT SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0018    5    NOT SELECTED

Posted By Unknown12:08

Monday 13 October 2014

TAMKO LA WAKRISTO BUKOBA KUHUSIANA NA MAUAJI PAMOJA NA UCHOMAJI WA MAKANISA

Filled under:

TAMKO LA WAKRISTO BUKOBA KUHUSIANA NA MAUAJI PAMOJA NA UCHOMAJI MAKANISA TAREHE 11/10/2014.


Baada ya tukio la kutisha la kushambuliwa kwa washirika na hatimaye kuuawa kwa mshirika na kujeruhiwa vibaya kwa mwingine kanisani Kagemu PAG; Wachungaji na viongozi wa kiroho wa Bukoba tumepokea taarifa hizi kwa mshtuko mkubwa. Tumekutana tarehe 10 Oct 2014 na kutafakari hatima ya wakristo katika eneo hili.

Matukio rejea tuliyojikumbusha ni kama ifuatavyo:

1. Kanisa la Living water pale Buyekera mlimani limechomwa moto mara.

2. Kanisa la Hofan ministries limechomwa moto pale Rugambwa.

3. Kanisa la la International assemblies of God lilipo Magoti lilichomwa moto na kuteketea.

4. Kanisa la TAG Kihwa lilichomwa moto na kuteketea.

5. Makanisa mengine maeneo ya vijijini kuchomwa moto nayo ni pamoja na Ruhanga TAG, Kakindo PAG na Kasharu EAGT.

6. Vitisho na Kushambuliwa kwa mawe wakati ibada zikiendelea mara kwa mara Kanisa la PAG Buyekera.

7. Kanisa la EAGT Kibeta kushambuliwa kwa mawe baada ya kundi la watu kuvamia kanisani miezi 3 iliyopita

8. Kanisa la Harvest kushambuliwa kwa mawe usiku na kundi la watu.

9. Jaribio la kuchomwa kisu Askofu Sesse Lazaro wakati akiwa kanisani.

10. Kifo cha kutatanisha cha Mch Jackson Kabuga wa TAG Kashabo.

Mengi ya matukio haya yameripotiwa katika vyombo vya usalama ingawa hatujapata mrejesho wowote toka vyombo hivi.

Kwa mtazamo wetu huu ni mpango uliolasimishwa wa kujenga hofu na hatimaye kukomesha uhuru wetu katika kumwabudu Mungu. Matukio haya japo yanaonekana hayahusiani lakini yamebeba maudhui inayofanana na yanatekelezwa kwa mbinu zinazofanana na inawezekana na kundi moja lenye mtandao mpana.

Kwa tamko hili tunataka yafuatayo yazingatiwe:

a. Kwa hali hii wakristo tutaweka mtandao unaojitegemea wa ki ulinzi wa nyumba za ibada, viongozi wa kiroho, na washirika wetu pamoja na hatua nyingine zozote za kiusalama tutakazoona zinafaa.

b. Tunaitaka serkali ifanye uchunguzi wa kina juu ya tukio hili na mengine yaliyotangulia na kutupatia taarifa ndani ya muda mfupi juu ya mafanikio au kukwama kwa uchunguzi.

c. Kwa Wakristo wote walioguswa na kuumizwa na tukio hili maneno la Mungu toka Rumi 8:37-39 yawe faraja yetu:

“Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda. Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.” Amen

Tamko hili limetolewa na Wachungaji 35 waliokaa katika kikao cha dhararula PAG tarehe 10/10/2014 na kutiwa sahihi kwa niaba yao na:-

Mch Crodward Edward.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wachungaji Bukoba.

Posted By Unknown04:18

Tuesday 7 October 2014

ALIYEBADILI JINSIA ASHINDA KESI

Filled under:


Audrey amekuwa akitaka baraza la mitihani kubadili jina lake na utambulisho wake wa kijinsia
Mwanamke aliyebadili jinsia yake ya kiume na kuwa mwanamke na kutaka jina lake kubadilishwa kwenye cheti chake cha mtihani ameshinda kesi yake dhidi ya baraza la kitaifa la mitihani nchini Kenya.

Mahakama imelazimisha baraza hilo kumpa Adrey Mbugua cheti kipya kinachoonyesha hali yake mpya ya kijinsia hasa kwa kuwa anapokea matibabu ya kufanikisha jinsia yake kubadilika kabisa.

Bi Mbugua alilishitaki baraza la kitaifa la mitihani nchini humo kwa kukataa kubadililisha utambulisho wa jinsia yake kwenye cheti hicho kutoka kwa Mwanamme na kumtambua kama mwanamke licha ya amri iliyotolewa katika gazeti rasmi la serikali.

Jaji Weldon Korir amelipatia baraza hilo hadi siku 45 kubadilisha jina la Adrey katika cheti hicho kutoka kwa 'Andrew Mbugua' na utambulisho wa mwanamume na kulibadilisha kuwa jina la kike la 'Audrey Mbugua' bila ya kuweka jinsia yoyote.

Jaji alisema kuwa jinsia ya Adrey kwenye cheti hicho haiongezi thamani yoyote kwa matokeo yake wala alama alizopata Audrey na kuondolewa kwake vile vile hakuna athari yoyote.

Aliongeza kuwa Audrey ameonyesha kuwa yuko tofauti na hivyo ndivyo anavyopaswa kutambuliwa.
'Audrey ni mwanadamu ambaye anajitambua kwama mwanamke wala sio kama mwanamume jinsia aliyozaliwa nayo,'' alisema jaji.

Jaji alisema kuwa katiba ya nchi inaamrisha watu kuwaheshimu wengine kama ipasavyo bila ubaguzi wowote na kwamba heshima hiyo inahusu mambo mengi ikiwemo mtu anavyotaka kutambuliwa.

Aliongeza kuwa ili Audrey kuhisi kuwa sawa anapaswa kukubalika kama alivyo na kumyima haki hiyo ya kubadilisha jina lake katika chati chake itakuwa ukiukwaji wa haki zake za kibinadamu.

Wakili wa Audrey, aliambia mahakama kuwa mteja wake alizaliwa na kasoro ya kijinsia na kwamba anaendelea kupokea matibabu.

Posted By Unknown10:08

MDEE NA WENZAKE WASOTEKWA SEGEREA

Filled under:



Mbunge wa Kawe na Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Halima Mdee.

Mbunge wa Kawe na Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Halima Mdee na wenzake tisa wamepelekwa katika Gereza la Segerea jijini Dar baada ya kushindwa kutimiza baadhi ya masharti ya dhamana yao.

Mdee na wenzake nane mapema leo walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar na kukana tuhuma zinazowakabili.

Mdee na wenzake hao wanashitakiwa kwa makosa mawili kototii amri za maofisa wa polisi na kufanya maandamano kinyume na sheria Jumamosi iliyopita ya Oktoba 4, mwaka huu.
Watapandishwa tena kizimbani hapo kesho saa 4 asubuhi.


(Habari na Deogratius Mongela/GPL

Posted By Unknown09:59