Thursday 30 October 2014

AJIRA: MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO TANZANIA AUTOMOTIVE TECHNOLOGY CENTRE

Filled under:

MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO OFFICE ASSISTANT - NYUMBU
WASAILIWA WALIOFANIKIWA KUENDELEA NA USAILI WA MAHOJIANO, MAHALI: NYUMBU - KIBAHA TAREHE 30-10-2014 SAA MOJA KAMILI ASUBUHI.
KADA: OFFICE ASSISTANT

EXAMINATION NUMBES    SCORE    REMARKS
PSRS NYUMBU OA 0022    55    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0042    55    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0024    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0028    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0036    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0041    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0004    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0034    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0039    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0050    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0014    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0017    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0031    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0005    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0006    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0047    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0001    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0002    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0010    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0019    50    SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0023    40    NOT SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0027    40    NOT SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0048    40    NOT SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0012    35    NOT SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0052    35    NOT SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0037    35    NOT SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0045    35    NOT SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0009    5    NOT SELECTED
PSRS NYUMBU OA 0018    5    NOT SELECTED

Posted By Unknown12:08

Monday 13 October 2014

TAMKO LA WAKRISTO BUKOBA KUHUSIANA NA MAUAJI PAMOJA NA UCHOMAJI WA MAKANISA

Filled under:

TAMKO LA WAKRISTO BUKOBA KUHUSIANA NA MAUAJI PAMOJA NA UCHOMAJI MAKANISA TAREHE 11/10/2014.


Baada ya tukio la kutisha la kushambuliwa kwa washirika na hatimaye kuuawa kwa mshirika na kujeruhiwa vibaya kwa mwingine kanisani Kagemu PAG; Wachungaji na viongozi wa kiroho wa Bukoba tumepokea taarifa hizi kwa mshtuko mkubwa. Tumekutana tarehe 10 Oct 2014 na kutafakari hatima ya wakristo katika eneo hili.

Matukio rejea tuliyojikumbusha ni kama ifuatavyo:

1. Kanisa la Living water pale Buyekera mlimani limechomwa moto mara.

2. Kanisa la Hofan ministries limechomwa moto pale Rugambwa.

3. Kanisa la la International assemblies of God lilipo Magoti lilichomwa moto na kuteketea.

4. Kanisa la TAG Kihwa lilichomwa moto na kuteketea.

5. Makanisa mengine maeneo ya vijijini kuchomwa moto nayo ni pamoja na Ruhanga TAG, Kakindo PAG na Kasharu EAGT.

6. Vitisho na Kushambuliwa kwa mawe wakati ibada zikiendelea mara kwa mara Kanisa la PAG Buyekera.

7. Kanisa la EAGT Kibeta kushambuliwa kwa mawe baada ya kundi la watu kuvamia kanisani miezi 3 iliyopita

8. Kanisa la Harvest kushambuliwa kwa mawe usiku na kundi la watu.

9. Jaribio la kuchomwa kisu Askofu Sesse Lazaro wakati akiwa kanisani.

10. Kifo cha kutatanisha cha Mch Jackson Kabuga wa TAG Kashabo.

Mengi ya matukio haya yameripotiwa katika vyombo vya usalama ingawa hatujapata mrejesho wowote toka vyombo hivi.

Kwa mtazamo wetu huu ni mpango uliolasimishwa wa kujenga hofu na hatimaye kukomesha uhuru wetu katika kumwabudu Mungu. Matukio haya japo yanaonekana hayahusiani lakini yamebeba maudhui inayofanana na yanatekelezwa kwa mbinu zinazofanana na inawezekana na kundi moja lenye mtandao mpana.

Kwa tamko hili tunataka yafuatayo yazingatiwe:

a. Kwa hali hii wakristo tutaweka mtandao unaojitegemea wa ki ulinzi wa nyumba za ibada, viongozi wa kiroho, na washirika wetu pamoja na hatua nyingine zozote za kiusalama tutakazoona zinafaa.

b. Tunaitaka serkali ifanye uchunguzi wa kina juu ya tukio hili na mengine yaliyotangulia na kutupatia taarifa ndani ya muda mfupi juu ya mafanikio au kukwama kwa uchunguzi.

c. Kwa Wakristo wote walioguswa na kuumizwa na tukio hili maneno la Mungu toka Rumi 8:37-39 yawe faraja yetu:

“Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda. Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.” Amen

Tamko hili limetolewa na Wachungaji 35 waliokaa katika kikao cha dhararula PAG tarehe 10/10/2014 na kutiwa sahihi kwa niaba yao na:-

Mch Crodward Edward.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wachungaji Bukoba.

Posted By Unknown04:18

Tuesday 7 October 2014

ALIYEBADILI JINSIA ASHINDA KESI

Filled under:


Audrey amekuwa akitaka baraza la mitihani kubadili jina lake na utambulisho wake wa kijinsia
Mwanamke aliyebadili jinsia yake ya kiume na kuwa mwanamke na kutaka jina lake kubadilishwa kwenye cheti chake cha mtihani ameshinda kesi yake dhidi ya baraza la kitaifa la mitihani nchini Kenya.

Mahakama imelazimisha baraza hilo kumpa Adrey Mbugua cheti kipya kinachoonyesha hali yake mpya ya kijinsia hasa kwa kuwa anapokea matibabu ya kufanikisha jinsia yake kubadilika kabisa.

Bi Mbugua alilishitaki baraza la kitaifa la mitihani nchini humo kwa kukataa kubadililisha utambulisho wa jinsia yake kwenye cheti hicho kutoka kwa Mwanamme na kumtambua kama mwanamke licha ya amri iliyotolewa katika gazeti rasmi la serikali.

Jaji Weldon Korir amelipatia baraza hilo hadi siku 45 kubadilisha jina la Adrey katika cheti hicho kutoka kwa 'Andrew Mbugua' na utambulisho wa mwanamume na kulibadilisha kuwa jina la kike la 'Audrey Mbugua' bila ya kuweka jinsia yoyote.

Jaji alisema kuwa jinsia ya Adrey kwenye cheti hicho haiongezi thamani yoyote kwa matokeo yake wala alama alizopata Audrey na kuondolewa kwake vile vile hakuna athari yoyote.

Aliongeza kuwa Audrey ameonyesha kuwa yuko tofauti na hivyo ndivyo anavyopaswa kutambuliwa.
'Audrey ni mwanadamu ambaye anajitambua kwama mwanamke wala sio kama mwanamume jinsia aliyozaliwa nayo,'' alisema jaji.

Jaji alisema kuwa katiba ya nchi inaamrisha watu kuwaheshimu wengine kama ipasavyo bila ubaguzi wowote na kwamba heshima hiyo inahusu mambo mengi ikiwemo mtu anavyotaka kutambuliwa.

Aliongeza kuwa ili Audrey kuhisi kuwa sawa anapaswa kukubalika kama alivyo na kumyima haki hiyo ya kubadilisha jina lake katika chati chake itakuwa ukiukwaji wa haki zake za kibinadamu.

Wakili wa Audrey, aliambia mahakama kuwa mteja wake alizaliwa na kasoro ya kijinsia na kwamba anaendelea kupokea matibabu.

Posted By Unknown10:08

MDEE NA WENZAKE WASOTEKWA SEGEREA

Filled under:



Mbunge wa Kawe na Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Halima Mdee.

Mbunge wa Kawe na Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Halima Mdee na wenzake tisa wamepelekwa katika Gereza la Segerea jijini Dar baada ya kushindwa kutimiza baadhi ya masharti ya dhamana yao.

Mdee na wenzake nane mapema leo walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar na kukana tuhuma zinazowakabili.

Mdee na wenzake hao wanashitakiwa kwa makosa mawili kototii amri za maofisa wa polisi na kufanya maandamano kinyume na sheria Jumamosi iliyopita ya Oktoba 4, mwaka huu.
Watapandishwa tena kizimbani hapo kesho saa 4 asubuhi.


(Habari na Deogratius Mongela/GPL

Posted By Unknown09:59

Thursday 25 September 2014

HOTEL YA BLUE PEAR YA UBUNGO YAFUNGWA KISA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Filled under:

 
Fanicha za hoteli ya Blue Pearl viitolewa nje. (picha: The Citizen)
Huduma za hoteli ya Blue Pear ya Ubungo jijini Dar es Salaam imefungwa baada ya mmiliki kuripotiwa kushindwa kulipa fedha ya pango inayokadiriwa kufikia shilingi bilioni sita ($3,800,000).
Gazeti la The CITIZEN linaripoti kuwa juzi mchana maafisa wa kampuni ya Majembe Auction Mart walifika katika eneo la hoteli hiyo na kuanza kutoa fanicha nje kisha kuzipakia kwenye lori.
Wateja waliambiwa wahame kutoka kwenye eneo la hoteli hiyo kwa kuwa ilikuwa imefungwa na huduma kusitishwa.
Mr Seth Motto wa Majembe Auction Mart alisema kampuni yake ilipewa jukumu hilo na menejimenti ya Ubungo Plaza Ltd, ambao ni wamiliki wa jengo hilo.

Posted By Unknown23:50

VIPEPERUSHI VYENYE MANENO YA VITISHO VYASAMBAZWA DODOMA

Filled under:


WanaCCm walifika katika jengo lao leo Alhamisi, Septemba 25, 2014, Dodoma na kukuta limeandikwa maneno kwa rangi nyekundu "NO KATIBA UFISADI " na kama hilo halitoshi kukawepo vipepersuhi vinasambazwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME - SACP amesema tarehe 25/09/2014 alfajiri vimeokotwa vipeperushi maeneo mbalimbali mjini Dodoma vyenye ujumbe ufuatao: ONYO – DODOMA SI MAHALI PA KUFUGA WEZI WA FEDHA ZA UMMA. UTAKAYEINGIA BUNGENI KUANZIA KESHO, YATAKAYOKUPATA UTAJUTA.
Kamanda MISIME amesema tumeendelea kupokea taarifa za watu wanaodaiwa kuandaa vipeperushi hivyo na tunafanyia kazi ili tuweze kuwakamata ili washtakiwe kulingana na kosa walilolitenda hasa la kutoa vitisho na kuhamasisha uvunjifu wa amani.

Aidha Kamanda MISIME ameongeza ametoa wito kwa wananchi na wageni wanaofika Dodoma watii sheria bila shuruti. Kila mmoja ajiepushe kujiingiza kwenye kuhamasisha uvunjifu wa amani, kujiingiza katika mikusanyiko isiyo halali na maandamano ambayo yameshapigwa marufuku na Jeshi la Polisi.

Atakayekiuka na kujiingiza katika vitendo hivyo vya kiuhalifu atashurutishwa kwa nguvu zote kwa mujibu wa sheria za Nchi na kwa mamlaka iliyopewa Jeshi la Polisi.

Kamanda MISIME ameongeza kuwa wananchi na wageni wapenda amani waendelee na shughuli zao kama kawaida kwani Jeshi la Polisi limejiimarisha ipasavyo kukabiliana na yeyote yule atakayekiuka sheria na maelekezo yaliyotolewa.


  • Taarifa ya Sylvester Onesmo wa Jeshi la Polisi, Dodoma.

Posted By Unknown23:27

WARAKA WA MLIMANDAGO ALIVYOMCHAFUA DIALO KWA KUMLIPUA LOWASA

Filled under:

NAIBU Waziri wa zamani wa Maji, Anthony Diallo, amesema dhana inayojengwa kwamba Mradi wa Maji wa Ziwa Victoria ulifanikishwa kwa nguvu ya aliyekuwa Waziri, Edward Lowassa, ni potofu na afadhali angetajwa yeye.

Katika mazungumzo na Raia Mwema yaliyofanyika mjini Mwanza wiki hii na ambayo yatachapishwa katika gazeti dada la hili la Raia Tanzania kesho, Diallo ambaye sasa ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mwanza, ameweka wazi kwa kila hatua kuhusu mradi huo.

Kimsingi, Diallo ameeleza kwamba mradi huo wa maji ulitokana na ahadi iliyotolewa na Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, kwa wananchi wa Kanda ya Ziwa mwaka 2000 na kama ingekuwa sifa ni bora zingeenda kwake.

“Kwanza kuna vitu viwili. Cha kwanza miradi yote inayolipiwa na kodi za wananchi ni jukumu la serikali iliyoko madarakani, sidhani anaweza kutokea mtu mmoja kudai kwamba nilifanikisha hiki.
Ukienda kwa staili hiyo ndiyo watu wanasema ile dhana ya wabunge kuwa mawaziri inaleta haya matatizo kwamba mtu anavutia kwake akiwa na nia fulani, sasa hao wanaodai kwamba walifanya hivi definitely lazima ujue kwamba wana nia fulani, wanataka kuwavutia wapiga kura kwamba wao wanawajali sana.

Sitakueleza mambo ambayo ni siri ya Baraza la Mawaziri, siwezi kuitoa, lakini moja ni kwamba mradi huo ulikuwa ahadi ya Rais Mkapa, mwaka 2000 wakati anaomba kura kipindi cha pili, alipopita Shinyanga na Kahama alisema lazima tufanye chini juu tutajenga mradi wa maji kuelekea huko kutoka Ziwa Victoria.

Sasa ngoma ilikuwa ni pesa zitapatikana wapi, mwaka 2002 tukaanza mazungumzo makali sana na nchi hizi zilizo kwenye Bonde la Nile, na bahati nzuri mimi ndiye nilihudhuria vikao vyote, mpaka tukafika mahali tukauvunja ule mkataba wa Misri na Uingereza, kwa sababu walikuwa wanatuzuia tusitumie maji ya Ziwa Victoria na hiyo mikutano yote nimehudhuria mimi, Addis Ababa. Na nimshukuru sana waziri mwingine aliyenisaidia, maana nilikuwa vocal sana, Martha Karua wa Kenya, aliyekuwa Waziri wa Maji wakati huo,”

alisema Diallo.

Kauli hii ya Diallo ni ya kwanza kutamkwa hadharani kuhusiana na mradi huo ambao mara nyingi
umekuwa ukitajwa na wapambe wa Lowassa kuwa kati ya kete zake muhimu ndani ya chama chake kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwakani.

Wapambe hao wamekuwa wakisema ni Lowassa aliyeusukuma na kuusimamia tangia kwenye mchakato wa kuondoa tatizo la maji kwa wananchi wa Kanda ya Ziwa, hasa Shinyanga na Kahama.

Katika mazungumzo hayo, Diallo alieleza ya kuwa akiwa Naibu Waziri chini ya Lowassa, namna alivyoshiriki katika kila hatua kabla ya kuhamishwa wizara.

“Baada ya hapo ikaja ngoma kwamba huu mradi utapate pesa kutoka wapi. Mimi nikafanya utafiti mdogo nikagundua kwamba tusingeweza kupata hela za wahisani kokote kwa sababu World Bank (Benki ya Dunia) jamaa wa Misri wamejaa hata IMF (Shirika la Fedha Duniani) kote kule wamejaa.

Lakini pia tukakumbuka miaka ya 1960 tulipokazana kuchukua haya maji kwenye mradi ule wa Wendele, nchi za Scandinavia zikazuia kwamba tusichukue maji Ziwa Victoria badala yake wakasema tuchimbe malambo, yakaja matrekta mengi na kwa sababu tulikuwa hatuna ufundi matrekta hayo mengi yamekuja kukusanywa kwenye vyuma chakavu, kama unakumbuka kulikuwa na katapila karibu kila kijiji mengi yamekuja kukusanywa kama vyuma chakavu. Kwa hiyo ilikuwa ni tabu sana pesa mtapata wapi.

Nikaja na wazo kwamba kwanini tusiombe pesa kwa Rais, tutumie pesa zetu wenyewe, wakati huo pesa za makusanyo ya kodi zilianza kupanda sana. Basi tukamwandikia barua Rais, tukamwambia uwezekano wa kupata funding ni mdogo sana, kwa hiyo akakubali tutumie pesa zetu wenyewe.

Wakati ule huo mradi ulikadiriwa kumalizika kwa bilioni 27. Mimi nikaja na wazo pale wizarani, nikawaambia kwa pesa hiyo huu mradi hauwezi kuisha , kwanini tusilishawishi Baraza la Mawaziri tufanye kwa awamu, tukaandika mradi wetu na matarajio yote tukakubaliwa.

Ili tujenge kwanza pampu na lile tenki la Ihelele (kijiji kando ya ziwa unakoanzia mradi huo) hiyo ilikuwa awamu ya kwanza bilioni 27 zingeishia hapo. Nikawa nawatania wizarani kwamba tukishafikisha maji pale (Ihelele) hakuna Wizara itakayopinga tusichukue hela kuyapeleka maji mbele.

Awamu ya pili ilikuwa umeme tutaupata wapi, kwa sababu pale (kwenye chanzo cha maji) ni porini tu, mara ya kwanza tukakubaliana kwamba tujenge sub station (kituo kidogo) lakini Tanesco hawakuwa waangalifu sana ule mradi tukaliwa, kwa sababu waliweka nguzo na nyaya ambazo ni sub standard (chini ya kiwango) zisingeweza kuendesha yale mapampu.

Tukaja na wazo la kuchukua umeme Kahama Mining, ikadibi tufanye hivyo, zile nguzo za awali zikatelekezwa. Hapo serikali tulikula hasara, ingawa si mbaya kwa sababu tulikuwa tunafanya kitu kinaitwa learning curve na watalamu wetu hawakuwa wazuri kiasi hicho.

Idea ya pili niliyoitoa mimi, nilikuwa mtu wa kwanza kuleta ule utaratibu wa design and build, nikawaambia hapa tukitaka tuweke feasibility study (upembuzi yakinifu), tutazeekea hapo mradi hautakamilika.

Kwa hiyo mkandarasi tutakayempa atakuwa ana design, tunaipitia design (michoro) yake na consultant (mtaalam mshauri) tutakuwa tumeshamuweka tunakubaliana anajenga ili mradi tunajua bei haiwezi kuvuka hapo.

Hata mkimuuliza Waziri Lowassa (Edward Lowassa Waziri wa Maji wakati huo) anakumbuka. Ule mradi ulikuwa mikononi mwangu, yeye alikuwa anashughulikia DAWASA. Tulikubaliana kugawana mimi nisimamie mradi wa Shinyanga yeye asimamie DAWASA, nilikuwa na maamuzi yote.

Huo mradi ndiyo ulikuwa hivyo, lakini ku- single out (huwezi kusema) kwamba nani aliukubali au aliukataa, ninajua waliokuwa wanaupinga lakini siwezi kusema ni nani kwa sababu ilikuwa ni siri, uamuzi wa Baraza la Mawaziri ni siri,” 
alisema Diallo.

Septemba mwaka jana, Lowassa alinukuliwa katika vyombo vya habari akieleza kwamba wakati alipopendekeza mradi huo wa maji kwenye Baraza la Mawaziri wakati wa enzi ya Mkapa, ni mawaziri wawili tu ndiyo waliomuunga mkono.

Akizungumza katika Kanisa la AICT mjini Kahama, Shinyanga, Lowassa alinukuliwa akiwataja mawaziri waliomuunga mkono kuwa ni Jakaya Kikwete ambaye alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakati huo na Muhammed Seif Khatib aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Muungano).




Katibu mwenezi mkoa wa Shinyanga ndugu Emmanuel Mlimandago


Posted By Unknown23:15