Thursday 25 September 2014

HOTEL YA BLUE PEAR YA UBUNGO YAFUNGWA KISA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Filled under:

 
Fanicha za hoteli ya Blue Pearl viitolewa nje. (picha: The Citizen)
Huduma za hoteli ya Blue Pear ya Ubungo jijini Dar es Salaam imefungwa baada ya mmiliki kuripotiwa kushindwa kulipa fedha ya pango inayokadiriwa kufikia shilingi bilioni sita ($3,800,000).
Gazeti la The CITIZEN linaripoti kuwa juzi mchana maafisa wa kampuni ya Majembe Auction Mart walifika katika eneo la hoteli hiyo na kuanza kutoa fanicha nje kisha kuzipakia kwenye lori.
Wateja waliambiwa wahame kutoka kwenye eneo la hoteli hiyo kwa kuwa ilikuwa imefungwa na huduma kusitishwa.
Mr Seth Motto wa Majembe Auction Mart alisema kampuni yake ilipewa jukumu hilo na menejimenti ya Ubungo Plaza Ltd, ambao ni wamiliki wa jengo hilo.

0 comments:

Post a Comment