Monday 24 March 2014

KINGUNGE:NILIWAHI KUVULIWA WADHIFU WA UKUU WA MKOA

Filled under:



MJUMBE wa Bunge Maalumu la Katiba, Kingunge Ngombere-Mwiru, alisema kuwa aliwahi kuvuliwa wadhifa wa ukuu wa mkoa kwa sababu ya kutofautia kimtazamo na hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.

Kingunge ambaye anawakilisha kundi la waganga wa tiba asili, alikumbushia tukio hilo juzi katika semina ya waandishi wa habari iliyofanyika mjini hapa katika Ukumbi wa Msekwa, naye akiwa mmoja wa watoa mada.

Akijibu swali la mwandishi wa gazeti hili la kwanini amegeuka mlalamishi wa kukosoa viongozi wenzake wa sasa wakati amekuwa sehemu ya serikali kwa awamu zote nne bila kutimiza wajibu wake, Kingunge alisema kuwa amekuwa akikosoa na wakati fulani iliwahi kumgharimu.

“Wakati fulani nikiwa mkuu wa mkoa, nilipingana na Mwalimu Nyerere nikikataa katiba isibadilishwe kwa manufaa ya watu fulani, basi nikafukuzwa ukuu wa mkoa. Hivyo si kweli kwamba sikukosoa, hata sasa naendelea,” alisema.

Katika mada yake kuhusu mapendekezo ya rasimu ya Katiba mpya, alisema kuwa nchi zinazopata fursa ya kuandika upya katiba zake, zinapaswa kujikita kuandika katiba bora zitakazoweza kuwa na misingi ya kukuza uchumi wa kujitegemea.

“Maisha yetu yameegemea uamuzi wa wenzetu. Tumepigania uhuru ili tujitawale lakini bado ni tegemezi na kama nchi iko hivyo halafu nafasi ya kuandika Katiba mpya inakuja mnapanga safu za vyeo haina maana,” alisema

0 comments:

Post a Comment