Saturday 30 November 2013

MENEJA NMB ABULUZWA KORTINI AKIDAIWA KUIBA SH48 MIL

Filled under:



Meneja wa Benki ya NMB  Ilala,  Gasper Urassa (49) amefikishwa Mahakama ya Wilaya ya Ilala kujibu shtaka la wizi wa Sh48 milioni.

Urasa alifikishwa katika mahakama hiyo kujibu shtaka linalomkabili la wizi wa Dola   30,000 za Marekani, mali ya Kampuni ya Epoch Mining Tanzania.

Wakili wa Serikali, Ester Martin alidai mahakamani hapo kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Novemba 11, mwaka huu katika benki ya NMB iliyopo Ilala.

Martin alidai siku ya tukio  kwenye benki  hiyo,  mshtakiwa aliiba Dola 30,000 za Marekani (Sh48 milioni) mali ya Kampuni ya  Epoch Mining Tanzania.

Mshtakiwa alikana shtaka na Hakimu Janeth Kinyage aliahirisha kesi hiyo hadi Desemba 10, mwaka huu itakapotajwa.
Mshtakiwa alirudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana ya kuwa na wadhamini wawili wa kuaminika, watakao saini hati ya Sh22.5 milioni.

0 comments:

Post a Comment