Saturday 30 November 2013

IMEBAINIKA VIDONGE VYA UZAZI WA MPANGO VINASABABISHA UPOFU

Filled under:







Pamoja na kuwa ni njia nzuri ya kuzuia ujauzito, vidonge vya Uzazi wa Mpango vinatajwa kusababisha  ugonjwa wa macho ujulikanao kama Glaucoma, unaoelezwa kuwa ni chanzo kikuu cha upofu.

Ugonjwa huu unaelezwa kuwa sababu kubwa ya kusababisha upofu kwa wanawake wanaotumia vidonge hivi kwa muda mrefu.

Hayo yamebainishwa kwenye Utafiti wa  Afya na Lishe  uliofanywa na Kituo cha Udhibiti na Uzuiaji wa Magonjwa cha Marekani(CDCP).

Utafiti huo unasema kuwa, seli zilizoko katika neva za macho zina homoni za estrogen  ambazo hufanya kazi ya kulinda macho, vidonge hivyo huingilia mchakato  huo wa ulinzi kwa kupunguza kiwango cha homoni hizo.

Unasema kuwa wanawake wanaofunga hedhi mapema au wanaotumia vidonge ambavyo huzuia kuzalishwa kwa vichocheo vya estrogen, na dawa za saratani ya matiti, huweza kupata upofu.
Wanawake zaidi  ya 3,400  wenye umri wa zaidi ya miaka 40 walifuatiliwa kwa zaidi ya miaka mitano ikiwa ni sehemu ya utafiti huo.

Profesa Shan Lin wa Chuo Kikuu cha Carlifonia, San Francisco anasema wanawake wanaotumia vidonge hivyo kwa zaidi ya miaka mitatu, wanatakiwa kupima maradhi ya macho aina ya Glaucoma na afya zao zifuatiliwe kwa uangalifu na wataalamu wa macho.

Utafiti huo umebaini kuwa wanawake waliotumia vidonge hivyo kwa miaka zaidi ya mitatu walikuwa na hatari kwa asilimia tano ya kupata upofu usababishwao na glaucoma ukilinganisha na wasiotumia vidonge  hivyo.

 Kiongozi wa utafiti huo, Dk Louis Pasquale  wa Chuo Kikuu cha Tiba cha Havard anasema vichocheo vya Estrogen  vina umuhimu katika  seli za retina ambazo zinajulikana kwa kupokea homoni hizo.
“Kuwepo kwa homoni za estrogen kunazisaidia seli hizo kuwa hai kwa hiyo wanawake wanapotumia vidonge vya uzazi, homoni hizo huharibiwa na kurahisisha uharibifu wa macho,” anasema Dk Pasquale.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake, Dk Cyriel Masawe wa Chuo  Kikuu cha Tiba cha Muhimbili (MNH) anasema  ni hatari kwa wasichana wadogo ambao hawajaolewa kutumia dawa hizo ovyo.
“Kwa mfano mikoa ya Lindi na Mtwara, tumegundua wasichana wadogo ambao hawajaolewa wanatumia zaidi sindano za uzazi wa mpango na vidonge,” anasema

0 comments:

Post a Comment