Monday 28 July 2014

TAARIFA ZILIZOTOLEWA HIVI KARIBUNI KUHUSU UGONJWA WA DENGUA

Filled under:

Gazeti la Mwananchi limechapisha habari kuwa kasi ya kuenea kwa homa ya dengue hapa nchini imepungua baada ya taarifa kuonyesha kuwa hakuna mgonjwa mpya kuanzia Julai 15.
Dk Vida Mmbaga, mtaalamu wa Kitengo cha Epidemiolojia cha Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, alisema kasi ya kuenea kwa ugonjwa huo ambao umeathiri watu 1384, inaendelea kupungua.

Alisema hadi sasa hakuna mgonjwa aliyelazwa wala kubainika kuwa virusi vya ugonjwa huo.

Alisema hii ni mara ya tatu kwa homa ya dengue kuibuka nchini. Mara ya kwanza ilikuwa Julai 2010, Juni 2013 na mwaka huu ambao umesababisha madhara zaidi.

Dk Vida alisema tangu kutokea kwa ugonjwa huo ni watu wanne tu kutoka Dar es Salaam waliopoteza maisha.

0 comments:

Post a Comment