Thursday 22 May 2014

TAARIFA YA BAVICHA ILIYOTOLEWA KUHUSU UKAWA

Filled under:

TAARIFA KWA UMMA

UPOTOSHWAJI NA PROPAGANDA CHAFU DHIDI YA CHADEMA/UKAWA NA KIKUNDI KILICHOJIVIKA VYEO HEWA


Zimetolewa taarifa kwenye vyombo mbalimbali vya habari na mtu anayejitambulisha kwa jina la Fikiri Migiyo na ambaye amejitambulisha pia kama Mwenyekiti wa Mabaraza ya kanda ya Ziwa Magaharibiinayojumuisha mikoa ya Mwanza, Simiyu, Kagera na Geita akipinga kuundwa kwa umoja wakutetea katiba ya wananchi (UKAWA)

Aidha mtu huyo anayejitambulisha na BAVICHA ameenda mbali kwa kutoasiku 14 kwa CHADEMA kujiondoa kwenye UKAWA na pia kulaani kitendo cha UKAWA kususia Bunge la Katiba.

Barazala Vijana wa Chama cha Demokrasisa na Maendeleo (CHADEMA) linapenda kuufahamisha umma wa Tanzania na wapenda mabadiliko mambo yafuatayo:-

1. BAVICHA haina kiongozi wa jina hilo la Fikiri Mayingi kwa Mkoa wa Geita 

2. Katika muundo wa chama na Mabaraza yake hakuna cheo kinachoitwa Mwenyekiti wa makatibu wa Mabaraza kwa Kanda. Hivyo mtu huyo aliyetoa tamko hilo amejipachika cheo hicho ili kukidhi hajana matakwa yake binafsi kwa nia ovu ya kuichafua CHADEMA 

3. Pia ni muhimu umma ukaelewa kuwa Muundo wa uongozi wa BAVICHA na hata mabaraza mengine ya chama unakomea kwenye ngazi ya mkoa na kisha Taifa mpaka hapo muundo wa kanda utakapohuishwa kwenye mfumo wa baraza kuanzia kwenye chaguzi zijazo. Hivyo kilichotolewa kwa umma ni cha kuupuuza.

4. BAVICHA haijawahi kufanya uchaguzi kwa mikoa yote mipya ya Geita, Simiyu, Njombe na Katavi hivyo kusema kwamba yeye ni mwenyekiti wa makatibu wa mabaraza ya chama kwa mikoa tajwa ni hila za kisiasa zinazoendeshwa na kundi la vijana waasi wanaoendeshwa na kivuli cha mtu badala ya itikikati, falasafa na sera za CHADEMA.

5. Aidha, mkoa wa Simiyu uliotajwa kwenye taarifa ya mpotoshaji huyo kuwa ipo kanda ya Ziwa Magaharibi si sahihi licha ya kwamba tu haina uongozi wa BAVICHA zaidi ya Kamati ya Msukomo kwa masuala yote ya kichama ikiwemo mabaraza. Mkoa wa Simiyu uko kanda ya Ziwa Mashariki na si ziwa Magharibi kama alivyosema mpotoshaji.

6. Ieleweke kuwa, Hakuna Mwanachadema mwenye akili timamu anayeweza kupinga uwepo na shughuli za UKAWA kwenye mchakato huu wa katiba mpya, umoja unaobeba maslahi mapana ya taifa letu, umoja unaotete maoni ya wanachi dhidi ya wapinga maoni ya wananchi anaye jitambullisha kama mwanachadema, wanaopinga maoni ya wananchi na rasimu ya katiba mpya wanajulikani.

7. Aidha, hakuna mwanachadema/ BAVICHA mwenye akili timamu anayeweza kuunga mkono vitendo vya kibaguzi, kidini na kikabila, achilia mbali matusi na vitisho vilivyofanywa na Serikali na Wabunge wa CCM kwenye bunge la katiba kwa kupinga kitendo cha UKAWA kutoka nje ya bunge hilo. Mwanachadema anayeweza kutetea vitendo hivyo anajinasibisha kwa utambulisho wa CHADEMA lakini si mwanachadema.

8. Baraza la vijana la chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA) linawaomba wanachama na Watanzania kuwapuuza vijana hao wanao tumika kwa kujipachika vyeo visivyokuwepo hata kwenye Katiba ya Chama na Mabaraza yake ili kukidhi adhima na nia ovu ya kuchafua taswira nzima ya CHADEMA.

9. BAVICHA daima itaendelea kuunga mkono juhudi za UKAWA za kupigania upatikanaji wa Katiba bora ya Wanatanzania inayotokana na maoni yao wenyewe.

Imetolewa leo Jijini Dar es salaam na:
Deogratias Munishi
Katibu Mkuu - BAVICHA

0 comments:

Post a Comment