Tuesday 20 May 2014

MILIPUKO MIWILI YATOKEA KATIKA SOKO

Filled under:

Milipuko hiyo imetokea katika soko ambalo lina shughuli nyingi na ambalo lilikuwa na msongamano wa watu eneo la Kati mwa Nigeria.

Mwandishi wa BBC Ishaq Khalid aliye mjini humo anasema kuwa kuna hofu ya watu wengi kujeruhiwa hasa kwa kuwa soko hilo lilikuwa na idadi kubwa ya watu.

Haijulikani kilichosababisha milipuko hiyo mjini Jos, mji ambao umeshuhudia mashambulizi makali kati ya wakristo na waisilamu.

Kundi la Boko Haram, pia limekuwa likifanya mashambulizi katika mji huo.

0 comments:

Post a Comment