Monday, 13 January 2014

NDESAMBURO KUMBOOST LOWASA

Filled under:



 Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo amekitaka Chama Cha Mapinduzi (CCM), kiache kumsakama Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa kwa sababu tu ya kutaka kutimiza ndoto yake.
 
Ndesamburo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema Mkoa Kilimanjaro, alisema kama ni kuonyesha nia wapo wanachama wengine wa CCM wamefanya hivyo bila kusakamwa.
Lowassa anatajwa kuwa miongoni mwa wanaousaka urais mwaka 2015, na harakati zake hizo zinaonekana kuwakera baadhi ya viongozi wa CCM ambao wameanza kumwandama kwa maneno.
Tayari CCM kupitia kwa Makamu Mwenyekiti wake, Philip Mangula na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye wamekaririwa wakisema walioanza kampeni mapema watashughulikiwa.
Hata hivyo hakuna mahali popote ambapo Lowassa ambaye pia ni Mbunge wa Monduli amewahi kutangaza nia ya kuusaka urais isipokuwa amesema ana ndoto ambayo iko mbioni kutimia.
Akitoa salamu zake za mwaka mpya wa 2014 jana, Ndesamburo alisema si haki kila matamko ya viongozi wa CCM kumlenga Lowassa pekee wakati wapo wanachama wengine ndani ya CCM.
“Wanaotangaza nia mbona wako wengi sana huko CCM na wala siyo Lowassa peke yake,” alisema na kuongeza;
“Hao wanaomnyooshea kidole Lowassa hawa wengine hawawaoni?” alihoji Ndesamburo na kuwataka viongozi wa CCM kuacha unafiki na kuendesha mambo kwa “double standard” (ubaguzi).
Ndesamburo alisema ukimwondoa Lowassa, wapo wanachama wengine wa CCM wanaoshiriki kwenye harambee kanisani na misikitini, lakini hilo haliwagusi viongozi wa CCM isipokuwa Lowassa tu.
Mbunge huyo alisema njia pekee ya kuepukana na unafiki huo wa CCM ni kuichagua Chadema yenye malengo na maisha mazuri.

0 comments:

Post a Comment