Tuesday 17 December 2013

LEMA AIKALI KIDEDEA KAMATI YA BUNGE KUTOKANA NA KUTOZUNGUMZIA SUALA LA BOMU KWENYE MKUTANO CHADEMA

Filled under:



Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema ameeleza kushangazwa na hatua ya kamati ya Bunge kukwepa kuzungumzia suala la kurushwa bomu kwenye mkutano wa chama chake huko Arusha, Julai 15, mwaka huu.

Akichangia mjadala wa taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Ulinzi na ya Mambo ya Nje, bungeni jana, Lema alisema kamati hizo ziligusia suala la bomu lililorushwa kwenye Kanisa Katoliki Olasiti, Arusha na kuachana kuzungumzia lile la mkutano wa Chadema uliofanyika kwenye Viwanja vya Soweto.

Alisisitiza msimamo wa Chadema kuwa kinao mkanda wa video unaoonyesha mtu aliyelipua bomu Uwanja wa Soweto na kushangaa taarifa ya kamati hizo mbili kutokuzungumzia tukio hilo.
Alisema ushahidi huo ungewezesha vyombo vya ulinzi na usalama kumbaini mtu aliyerusha bomu hilo na kusisitiza kuwa wako tayari kukabidhi mkanda huo kwa tume huru itakayoundwa na Serikali kuchunguza tukio hilo.

Lakini bahati mbaya alikamatwa jambazi kule Nzega akapigwa ili anitaje mimi ndiye niliyerusha bomu Olasiti na nilipigiwa simu na mmoja wa ndugu wa jambazi huyo akaniambia kuhusu suala hilo... Tunao ushahidi nani alitaka kutuua, Serikali iunde tume tupeleke ushahidi wetu,” alisema.

Bomu katika uwanja huo lililipuka wakati Chadema kikihitimisha kampeni zake za udiwani katika Kata ya Kaloleni.
Mei 5, mwaka huu, watu wasiojulikana walirusha bomu katika mkusanyiko wa kidini katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasiti na kusababisha vifo vya watu watatu.

0 comments:

Post a Comment