
Watu sita wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika
shambulizi la kigaidi katika eneo la California mtaa wa Eastleigh,
mjini Nairobi.
Polisi wamesema kuwa milipuko miwili ilitokea
wakati magaidi waliporusha mabomu katika mkahawa mdogo ulio karibu na
kituo cha mabasi mtaani humo.
Walioshuhudia shambulizi walisema kuwa walisikia mlipuko wa tatu katika eneo hilo ingawa polisi hawajathibitisha...