Monday, 31 March 2014

SHAMBULIZI LA KIGAIDI LAUWA 6 NCHINI KENYA

Filled under:

Watu sita wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika shambulizi la kigaidi katika eneo la California mtaa wa Eastleigh, mjini Nairobi. Polisi wamesema kuwa milipuko miwili ilitokea wakati magaidi waliporusha mabomu katika mkahawa mdogo ulio karibu na kituo cha mabasi mtaani humo. Walioshuhudia shambulizi walisema kuwa walisikia mlipuko wa tatu katika eneo hilo ingawa polisi hawajathibitisha...

Posted By Unknown12:18

WALIMU YA AJIRA MPYA WALIOKUBALIWA KUBADILISHIWA VITUO 2014

Filled under:

WALIMU YA AJIRA MPYA WALIOKUBALIWA KUBADILISHIWA VITUO 2014 Ofisi ya Waziri Mkuu na Tawala  za Mikoa na Serikari za Mitaa imebadilishia vituo  kwa walimu wapya mwaka 2014 hii ni kutokana na maombi mbalimbali ya walimu hao,walimu waliokubaliwa ni pamoja na ngazi ya cheti,stashahada na shahada. Walimu wote walioomba kubadilishwa vituo waangalie majina yao katika orodha iliyotolewa na kama baadhi yao majina yao hawajayaona basi watambue...

Posted By Unknown11:24

JK AKIONGEA NA MAMIA YA WATANZANIA WAISHIO UINGEREZA

Filled under:

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia mamia ya Watanzania waishio Uingereza alipokutana nao usiku wa Machi 30, 2014 katika ukumbi wa Sattavis Patidar Centre, Wembley, London, Rais yupo katika ziara ya kiserikali ya  siku tatu kwa mwaliko wa Waziri Mkuu wa Uingereza Mhe David Camer...

Posted By Unknown06:24

KAMILI:MWENYEKITI WA CCM ALIHUSIKA KUNITESA

Filled under:

Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Rose Kamili, aliyedai ametekwa na kuteswa wakati wa uchaguzi mdogo mkoani Iringa, amemtuhumu Mwenyekiti wa CCM mkoani humo, Jessica Msambatavangu kuwa anahusika na mashambulizi dhidi yake.Kamili alidai alitekwa, kupigwa na kujeruhiwa wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Kalenga uliofanyika mapema mwezi huu. Akizungumza kwenye mkutano na wanahabari  mjini Dodoma, siku moja baada ya...

Posted By Unknown06:16

WATU WAWILI WAAMBUKIZWA EBOLA

Filled under:

  Ugonjwa huo umesemekana kutokana na Popo wanaoliwa kama kitoweo nchini Guinea  Watu wawili wameambukizwa ugonjwa hatari ya Ebola nchini Liberia ulioenezwa kutoka nchini Guinea ambako umewaua watu 78. Walioambukizana ugonjwa huo ni madada wawili, mmoja wao akiwa tu ndio amerejea kutoka nchini Guinea. Maafisa wanasema kuna wasiwasi kuwa ugonjwa huo unaendelea kuenea. ...

Posted By Unknown06:02

Friday, 28 March 2014

TAARIFA YA MBUNGE WA NZEGA KWA UMMA KUHUSIANA NA UPOTOSHAJI ULIOFANYWA NA TCME

Filled under:

Taarifa ya Mbunge wa Nzega kwa Umma Kuhusiana na Upotoshaji Uliofanywa na Taasisi ya Tanzania Chamber of Minerals and Energy (TCME) Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Nzega imesikitishwa na kufadhaishwa na taarifa ya uongo na isiyo na uzalendo hata chembe, iliyotolewa na taasisi ya TCME siku ya tarehe 26, Machi, 2014. Hii imedhihirisha kuwa, hawajui wanalolifanya ama wanatumiwa vibaya na watu wenye maslahi ovu kwa wachimbaji wadogo wadogo wa Nzega na wa Tanzania kwa Ujumla. Taarifa za namna hii hazina maksudi mengine zaidi ya kusababisha chuki...

Posted By Unknown08:43

NDEGE YA MALAYSIA KUTAFUTWA KATIKA ENEO JIPYA

Filled under:

  Ndege 9 za kijeshi na Moja ya kiraiya zinatafuta mabaki ya ndege ya Malaysia ya MH370 Maafisa wanaosaidia katika harakati za kuitafuta ndege ya Malaysia ya MH370 iliyopotea majuma tatu yaliyopita , wametangaza kuwa wanabadilisha eneo la kuitafuta mabaki ya ndege hiyo. Eneo hilo jipya litakuwa kilomita elfu moja mia moja kazkazini mashariki mwa kusini mwa bahari hindi. Mamlaka ya...

Posted By Unknown08:21

Tuesday, 25 March 2014

TANGAZO LA SERIKALI KUHUSU KUVUNJWA KWA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA

Filled under:

TANGAZO LA SERIKALI KUHUSU KUVUNJWA KWA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA Mhe. Rais aliunda Tume ya Mabadiliko ya Katika kwa mujibu wa kifungu cha 5 na 6 cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83 kwa Tangazo la Serikali Na.110 la Mwaka 2012. Tume ilikusanya maoni na kuandaa Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo imewasilishwa kwenye Bunge Maalum. Kwa mujibu wa kifungu cha 31 cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura...

Posted By Unknown08:37

MKURUGENZI WA BODI YA ATALII AVULIWA MADARAKA

Filled under:

Serikali imemvua wadhifa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Utalii nchini (TTB), Dk Aloyce Nzuki kutokana na utendaji usioridhisha. Akitangaza uamuzi huo jana mbele ya waandishi wa habari, Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu alisema kuwa ameridhia uamuzi wa bodi ya wakurugenzi wa shirika hilo ambao walipendekeza mkurugenzi huyo aondolewe. Katika barua waliyomwandikia Waziri ikiwa imesainiwa na...

Posted By Unknown08:31

KINGWANGALLA AKAMATWA NA POLISI KISA!!

Filled under:

JESHI la Polisi wilayani Nzega, mkoani Tabora limemkamata na kumuachia kwa masharti Mbunge wa Nzega, Dk. Hamis Kigwangallah, kwa madai ya kuongoza maandamano ya wachimbaji wadogo wa dhahabu ambao wanapinga kufungwa kwa machimbo ya Mwashina, yaliyo jirani na mgodi wa Resolute Tanzania Limited. Mbunge huyo alikamatwa majira ya saa 10:00 jioni juzi baada ya kufanya maandamano yasiyo na kibali yaliyoanza saa saba mchana. Kabla ya hapo...

Posted By Unknown08:22

Monday, 24 March 2014

KINGUNGE:NILIWAHI KUVULIWA WADHIFU WA UKUU WA MKOA

Filled under:

MJUMBE wa Bunge Maalumu la Katiba, Kingunge Ngombere-Mwiru, alisema kuwa aliwahi kuvuliwa wadhifa wa ukuu wa mkoa kwa sababu ya kutofautia kimtazamo na hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere. Kingunge ambaye anawakilisha kundi la waganga wa tiba asili, alikumbushia tukio hilo juzi katika semina ya waandishi wa habari iliyofanyika mjini hapa katika Ukumbi wa Msekwa, naye akiwa mmoja wa watoa mada. Akijibu swali la mwandishi...

Posted By Unknown21:23

MKUMBO:UHALALI WA KITAFITI WA MAONI YA WANANCHI TUME YA WARIOBA

Filled under:

BUNGE la Katiba linatarajiwa kuanza kazi yake wiki hii baada ya kukamilisha na kupitisha kanuni zake na hatimaye kuchagua Mwenyekiti atakayeliongoza. Kazi kubwa ya Bunge hili ni kujadili na kupitisha Rasimu ya Katiba ambayo hatimaye itapigiwa kura na wananchi. Wabunge wana vigezo viwili vya kuwasaidia kufanya uamuzi wao katika ibara mbalimbali za rasimu inayopendekezwa na Tume ya Warioba. Kigezo cha kwanza ni kutumia kile tunachoweza...

Posted By Unknown21:12

MAMLAKA YA USALAMA WA SAFARI ZA BAHARINI YASITISHA SHUGHULI YA KITAFUTA MH370

Filled under:

  Jamaa za abiria wa ndege hiyo wamekumbwa na majonzi makubwa.                    Mamlaka ya usalama wa safari za baharini nchini Australia imesema kuwa operesheni ya kuitafuta ndege ya shirika la Malaysia iliyotoweka imesitishwa kutokana na hali mbaya ya hewa na mawimbi makali baharini. Taarifa zinasema kuwa upepo mkali pamoja na mvua kubwa inayonyesha...

Posted By Unknown20:56

WAZIRI WA MALAYSIA ASEMA NDEGE ILIDONDOKA BAHARI YA HINDI,HAKUNA ABIRIA ALIYESALIA

Filled under:

  Waziri mkuu wa Malaysia Najib Razak Shirika la ndege la Malaysia limewaambia jamaa na familia za abiria waliokuwa wanasafiri kwa ndege iliyotoweka MH370 kwamba ndege hiyo imepotea na kwamba hakuna manusura. Tangazo hilo limetolewa kwa familia hizo kwa njia ya ujumbe wa simu ya mkononi , ambao BBC iliweza kuuona. Ndege ya Malaysia MH320 ilitoweka ikiwa na abiria 239 baada ya kuruka...

Posted By Unknown11:49

ZIFAHAMU ATHARI ZA SABUNI ZITUMIKAZO KURUDISHA BIKIRA

Filled under:

KUWA mrembo ni pamoja na kujikubali jinsi ulivyo na jinsi utakavyojiweka soap soap Hata mtu akikupenda akupende  jinsi ulivyo.  Pamoja na hayo kumekuwa na mambo mbalimbali yanayofanywa na baadhi ya wanawake au wasichana kwa lengo la kufanikisha azma mbalimbali. Miongoni mwa mambo hayo ni matumizi ya madawa mbalimbali ikiwemo yake ya kuongeza hips, makalio, kubadilisha rangi ya ngozi na hata kufanyia operesheni sura ili kuwa na muonekano...

Posted By Unknown04:51

UMOJA WA WAKULIMA WA CHAI WAMBURUZA MAHAKAMANI JANUARY MAKAMBA

Filled under:

UMOJA wa Wakulima wa Chai (UTEGA) Halmashauri ya Bumbuli, wilayani Lushoto, Tanga unatarajia kumburuza mahakamani Mbunge wa Bumbuli, January Makamba. Uamuzi wa UTEGA ulitolewa hivi karibuni katika mkutano mkuu maalumu wa UTEGA ulioitishwa kwa nia ya kutathmini njia bora za kisheria za kuhakikisha kiwanda cha chai kinafunguliwa na kudai fidia ya athari walizopata kwa zaidi ya mwaka mmoja tangu kufungwa. Kwa mujibu wa UTEGA uamuzi...

Posted By Unknown04:31

BAADA YA KUBWAGANA NA RAY ,MAINDA APATA UJAUZITO

Filled under:

Siku chache baada ya kuliambia gazeti ndugu la hili, Amani kuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa chango hivyo inambidi azae, super lady wa sinema za Kibongo, Ruth Suka ‘Mainda’ anadaiwa kuwa mjamzito, Ijumaa Wikienda limechimba kila ‘engo’. MUONEKANO Habari zilieleza kwamba kimuonekano, Mainda aliyezoeleka kuonekana mwembamba, sasa ameanza kunenepa huku kitumbo nacho kikianza kuwa kikubwa. Habari kutoka kwa mmoja wa mashosti zake aliyeomba hifadhi...

Posted By Unknown03:32

HATUTAKUBALI KUJADILI RASIMU NYINGINE

Filled under:

  Bunge Maalumu la Katiba sasa lipo katika hati hati ya kuendelea kutokana na viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kutangaza kuwa hawatakuwa tayari kujadili rasimu tofauti na iliyowasilishwa na Jaji Joseph Warioba bungeni. Wakizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jana katika Ukumbi wa Pius Msekwa bungeni, viongozi wa Ukawa, Profesa Ibrahim Lipumba, James Mbatia, Freeman Mbowe na Tundu Lissu, walisema wataitetea...

Posted By Unknown03:02

BUNGE LA KATIBA KIZUNGUMKUTI

Filled under:

Kwa neno moja unaweza kusema kwamba wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba na wananchi kwa ujumla wako “njiapanda”. Hii ni baada ya hotuba ya ufunguzi wa Bunge hilo iliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete kuibua mambo mazito ambayo kimsingi yanatofautiana na mapendekezo yaliyomo katika Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa bungeni na mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba. Huku wananchi...

Posted By Unknown02:50