Tuesday, 29 July 2014

WABUNGE WA TANZANIA WAZITWANGA NGUMI KISA WIVU WA MAPENZI NCHINI MALAYSIA

Filled under:

Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wanadaiwa kupigana huko Malaysia baada ya kukutana hotelini, wakati wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), walipokuwa katika ziara ya kikazi nchini humo. Tukio hilo lilitokea siku nne zilizopita baada ya mbunge wa kamati hiyo kutoka CCM kuvamiwa alipokuwa akipata kifungua kinywa kwenye hoteli aliyofikia na wenzake wawili mmoja wa CCM na mwingine wa CHADEMA. Majina ya wabunge hao watatu tunayahifadhi kwa sasa kwa sababu hatukuwapata kujibu tuhuma hizo. Hata hivyo, mbunge...

Posted By Unknown01:06

SERIKALI YA TANZANIA YAZUIA AJIRA ZA IDARA YA UHAMIAJI

Filled under:

Serikali ya Tanzania  yazuia ajira za Idara  za Uhamiaji kwa madai ya upendeleo wa kindugu na kujuana....

Posted By Unknown00:42

WATUHUMIWA 10 WA UJAMBAZI WAKAMATWA NA SILAHA NZITO

Filled under:

  MAJAMBAZI 10 wanaounda mtandao hatari wa uhalifu nchini, wametiwa mbaroni wakati wa msako mkali uliofanikisha pia kukamatwa kwa silaha mbalimbali. Silaha hizo ni bunduki tisa zikiwemo SMG tatu, bastola mbili, short gun nne na risasi 15 zilikamatwa. Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, aliyasema hayo ofisini kwake kwenye mkutano na waandishi wa habari. Majambazi hao wamekamatwa katika msako mkali unaoendelea...

Posted By Unknown00:29

Monday, 28 July 2014

SIRI NZITO YAZIDI KUVUJA KUHUSU VIUNGO VYA BINADAMU

Filled under:

SIKU moja baada ya serikali kufunga Hospitali ya Chuo cha Kimataifa cha Matibabu na Teknolojia (IMTU), kwa madai ya kuendeshwa kwa kukiuka taratibu za tiba, Tanzania Daima Jumapili limedokezwa hatua hiyo imefikiwa ili kukinusuru chuo hicho na adhabu ya utupaji viungo vya binadamu. Kwamba uamuzi huo umefikiwa kutuliza hasira za makundi mbalimbali, kikiwamo Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), waliolaani utupaji huo. Wakati hatua...

Posted By Unknown02:27

KATIBA MPYA:WASSIRA,LIPUMBA NA LISSU WACHUANA VIKALI

Filled under:

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Uhusiano na Uratibu, Stephen Wassira akiwakilisha CCM, Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, jana walitoana jasho katika mdahalo wa Katiba ulioandaliwa na East African Business and Media Institute. Mdahalo huo uliohudhuriwa na watazamaji wapatao 500, ulikuwa na mada inayosema: ‘Nani anakwamisha Upatikanaji wa Katiba Mpya.’ Kila upande ulitumia fursa hiyo kutupa shutuma kwa mwingine huku jazba na kelele vikitawala miongoni mwa waliohudhuria. Hata hivyo,...

Posted By Unknown01:54

TAARIFA ZILIZOTOLEWA HIVI KARIBUNI KUHUSU UGONJWA WA DENGUA

Filled under:

Gazeti la Mwananchi limechapisha habari kuwa kasi ya kuenea kwa homa ya dengue hapa nchini imepungua baada ya taarifa kuonyesha kuwa hakuna mgonjwa mpya kuanzia Julai 15. Dk Vida Mmbaga, mtaalamu wa Kitengo cha Epidemiolojia cha Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, alisema kasi ya kuenea kwa ugonjwa huo ambao umeathiri watu 1384, inaendelea kupungua. Alisema hadi sasa hakuna mgonjwa aliyelazwa wala kubainika kuwa virusi vya ugonjwa huo. Alisema hii ni mara ya tatu kwa homa ya dengue kuibuka nchini. Mara ya kwanza ilikuwa Julai 2010,...

Posted By Unknown01:37

Thursday, 24 July 2014

MNADA WA HADHARA WA VIFAA VYA UBALOZI WA SWITZERLAND,FINILAND AND SWEDEN

Filled under:

UBALOZI WA SWITZERLAND, FINLAND & SWEDEN MNADA WA HADHARA: UNIVERSAL AUCTION CENTRE Kwa idhini waliyopewa na Ubalozi wa Switzerland, Finland & Sweden  watauza kwa mnada wa hadhara  Magari, Generators & Fanicha za Ofisi na nyumbani tarehe 26 July, 2014 Jumamosi saa 4.00 asubuhi. Mnada utafanyika Golden Resort Sinza,  Lion Street. MALI ZITAKAZOUZWA: Sofa sets, Dining Table & chairs, Coffee table, Book Shelves, Meza za ofisi/viti, File cabinets, Fridges, Cookers, TV set, Washer, Dryer, Camping Tents,...

Posted By Unknown10:58

NDEGE YA AIR ALGERIE IMEPOTEA IKIWA NA ABIRIA 116

Filled under:

Ndege ya Air Algerie imetoweka ikiwa na abiria 116 Shirika la ndege la Algeria , Air Algerie, limesema kuwa limepoteza mawasiliano na moja ya ndege zake ilipokuwa ikitoka mji mkuu wa Burkina Faso Ouagadougou. Afisa huyo anasema kuwa ndege hiyo ya Air Algerie ilikuwa imepaa dakika 50 katika anga ya Sahara mara ya mwisho mawasiliano yao. Ndege hiyo...

Posted By Unknown10:29

Wednesday, 23 July 2014

TIBA,KINGA YA UKIMWI YAGUNDULIKA

Filled under:

Watafiti katika Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba cha Temple, Marekani wamegundua dawa ya kuangamiza Virusi Vya Ukimwi (VVU) ambayo ni ya uhakika zaidi ukilinganisha na zilizowahi kupatikana katika tafiti za awali duniani.   Dawa yao inaweza kutumika kwa tiba ya wanaoishi na VVU na kinga kwa wale ambao bado hawajaambukizwa. Mmoja wa watafiti hao, Dk Kamel Khalili aliwaambia waandishi wa habari juzi mjini Philadelphia, Marekani kuwa tofauti na utafiti mwingine, wao wamegundua...

Posted By Unknown23:13

TAARIFA RASMI ILIYOTOLEWA NA POLISI KUHUSU KUTUPWA VIUNGO VYA BINADAMU MAENEO YA BONDE LA BWENI

Filled under:

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI JESHI LA POLISI TANZANIA PRESS RELEASE 22/07/2014 WATU WANANE WAKIWEMO MADAKTARI WASHIKILIWA NA KUHOJIWA NA JESHI LA POLISI KUTOKANA NA KUTUPWA VIUNGO VYA BINADAMU MAENEO YA BONDE LA MBWENI MPIJI ENEO LA BUNJU  Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linawashikilia watu wanane na kuwahoji kuhusu tukio la kupatina kwa viungo vya binadamu vilivyogundulika...

Posted By Unknown22:29

MTIKILA AENDA KORTINI KUOMBA AINGIZWE KWENYE KESI YA IPTL VS KAFULILA

Filled under:

MWENYEKITI wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila, ameomba kuunganishwa katika kesi ya madai inayomkabili Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila. Awali, Kafulila akizungumza kwenye mjadala katika eneo la Urusi Mwanga mjini Kigoma jana, alisema Mchungaji Mtikila ameomba kuwa mshitakiwa wa pili katika kesi hiyo huku Chama chake cha DP kikiwa mshitakiwa wa tatu. Pia alisisitiza kuwa kamwe hakukurupuka kuibua kashfa hiyo ya ufisadi katika akaunti ya Escrow na kwamba, yuko tayari kwa lolote. “Nimefarijika kuona wenzangu...

Posted By Unknown22:18

TAMKO LA CHADEMA KUHUSU KUONDOKA KWA WALIOKUWA VIONGOZI

Filled under:

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Jimbo la Kigoma Kaskazini tunapenda kutoa taarifa kwa umma kutokana na sintofahamu inayotaka kulazimishwa mbele ya jamii kuhusu uimara wa chama chetu mkoani Kigoma. Tangu jana na leo kumeenea taarifa zinazowahusu watu watatu, Jaffari Kasisiko, Msafiri Wamarwa na Mama Malunga Masoud, ambao vyombo mbalimbali vya habari vimeandika kuwa wamehama chama chetu cha CHADEMA na kukimbilia wanakojua wao (maana CCM inafanya kazi zake katika sura mbalimbali).Katika hatua ya awali, sisi CHADEMA Jimbo la Kigoma...

Posted By Unknown02:31

WATUMISHI WA NMB MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA KUUIBIA BENKI BILIONI 1

Filled under:

WATU watatu, akiwemo mtumishi wa Benki ya NMB, wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kujibu mashitaka 13, yakiwemo ya kuiibia benki hiyo zaidi ya sh. bilioni moja na kutakatisha fedha haramu. Mtumishi wa benki hiyo, Mtoro Suleiman, Daudi Kindamba na John Kikopa, walisomewa mashitaka hayo jana na Wakili wa Serikali Pius Hilla, mbele ya Hakimu Mkazi Hellen Riwa. Hilla aliwasomea washitakiwa hao mashitaka ya kula njama, kuiibia benki hiyo sh. 1,029,454,383, kufanya udanganyifu, kutakatisha fedha na kuisababishia...

Posted By Unknown01:48

TAARIFA YA MKURUGENZI WA UPELELEZI YA KUKAMATWA KWA WASHUKIWA 25

Filled under:

Kufuatia tukio la mlipuko wa bomu siku ya tarehe 7/7/2014 majira ya saa 22.15 usiku katika mgahawa wa VAMA, eneo la Uzunguni Jijini Arusha, ambapo watu wanane walijeruhiwa, Jeshi la Polisi limewakamata watuhumiwa 25 kwa uchunguzi. Kufuatia uchunguzi huo kati yao watu sita watafikishwa mahakamani mapema iwezakanavyo. Watuhumiwa watakaofikishwa Mahakamani kwa tukio hilo ni: SHAABAN MUSSA MMASA @ JAMAL, Umri miaka 26 Kabila, Msambaa. Mlinzi aliyekuwa zamu siku hiyo kwenye mgahawa huo.  Wengine ni ATHUMAN HUSSEIN MMASA, Umri miaka 38...

Posted By Unknown01:41