Friday, 18 April 2014

DIAMOND AFUNGIWA ASHINDWA KUMZIKA MZEE GURUMO

Filled under:

Kuna madai kwamba Nasibu Abdul ‘Diamond’ alishindwa kushiriki zoezi la kuuaga mwili wa mwanamuziki mkongwe Tanzania, marehemu Muhidin Mwalimu Mohamed Gurumo ‘Maalim Gurumo’ kwa sababu alifungiwa asitoke ndani na mwandani wake madam Wema Sepetu,   Wema Sepetu na Diamond wakiwa faragha. Imedaiwa kuwa, Wema alimfanyia ‘umafia’ mpenzi wake huyo, Aprili 15, mwaka huu ambapo ilikuwa ndiyo siku ya mwili wa marehemu huyo kuagwa nyumbani kwake Mabibo...

Posted By Unknown00:30

Thursday, 17 April 2014

UKAWA.HATURUDI BUNGE LA KATIBA

Filled under:

WAJUMBE  wa Bunge Maalumu, wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), wamesema hawatarudi bungeni na badala yake kuanzia kesho wataanza mikutano ya hadhara nchi nzima kuwaeleza wananchi juu ya hila za Chama Cha Mapinduzi (CCM) na washirika wake kutaka kuhodhi mchakato wa uandikaji wa Katiba mpya. UKAWA wamesema katika mikutano hiyo watazisambaza ‘CD’ zinazomuonesha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, akiwa katika Kanisa la Methodist, mkoani Dodoma akiwaeleza waumini wakatae muundo wa...

Posted By Unknown23:44

LUKUVI ALIKOROGA KWA CUF

Filled under:

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, amekiri kutoa maneno yanayodaiwa kuwa ya uchochezi kanisani kwa madai ya kuingiwa hofu na harakati za asasi ya kidini ya Uamsho, kufanana na za Chama cha Wananchi (CUF) za kudai Serikali ya mkataba. Waziri Lukuvi alitoa kauli hiyo jana bungeni, akitoa ufafanuzi wa kauli aliyopata kuitoa katika Kanisa la Methodist wakati wa kumsimika Askofu Mteule, Joseph Bundara. Katika...

Posted By Unknown23:25

UCHUNGUZI UMEBAINI NAHODHA MKUU WA FERI YA SOWEL HAKUWEPO KWENYE USUKANI

Filled under:

Waokoaji wamefaulu kuingia ndani ya feri iliyozama Naibu wa tatu wa nahodha wa ferri iliyozama ''Sewol'' ndiye aliyekuwa usukani wakati feri hiyo ilipozama. Uchunguzi wa kimsingi umebaini. Nahodha mkuu haijabainika alikuwa wapi wakati wa tukio ila inadhaniwa feri hiyo iligonga mwamba na kupinduka kwa haraka baada ya shehena yake kuegemea upande mmoja. ...

Posted By Unknown23:05

Wednesday, 16 April 2014

BUNGE LA KATIBA:UPINZANI WASUSIA KIKAO

Filled under:

Baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalum la Rasimu ya Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameondoka kwa hasira katika kikao cha bunge hilo kinachoendelea mjini Dodoma.  Hasira yao inatokana na madai kwamba maoni ya wananchi yaliyowasilishwa na Tume ya Marekebisho ya Katiba Mpya yamekuwa yakipuuzwa. Wajumbe wa bunge hilo ambao ni kutoka upande wa upinzani chini ya umoja unaojulikana kama UKAWA, yaani Umoja wa Katiba ya Wananchi, wameamua kutoka nje kupinga kile wanachosema ni...

Posted By Unknown10:10

KOREA KUSINI:WATU ZAIDI YA 300 BADO HAWAJAPATIKANA

Filled under:

Zaidi ya watu miatatu bado hawajapatikana baada ya meli iliyokuwa imewabeba wanafunzi kuzama nchini Korea Kusini. Awali maafisa walikuwa wamesema kuwa wengi wa abiria waliokuwa katika meli hiyo waliokolewa. Baadhi ya walionusurika wamekuwa wakielezea hali ilivyokuwa ya kutisha ndani ya meli ilipoanza kusimama kwa kuyumba, ikiegemea upande mmoja na haraka kuanza kuzama. ...

Posted By Unknown10:04

Monday, 14 April 2014

KITUO CHA MABASI CHALIPULIWA

Filled under:

Watu kadha wameripotiwa kuuawa nchini Nigeria kutokana na milipuko miwili iliyotokea katika kituo cha mabasi katika mji mkuu wa Nigeria, Abuja. Mwandishi wa BBC mjini Abuja, Haruna Tangaza anasema milipuko hiyo ilitokea wakati abiria wakiwa katika harakati za kupanda mabasi na teksi wakienda maofisini katikati ya mji wa Abuja. Watu walioshuhudia tukio hilo wanasema miili ya watu imetapakaa...

Posted By Unknown07:26

BUNGE LA KATIBA: MAONI YA WAJUMBE WALIO WACHACHE WA KAMATI NAMBA SITA YA BUNGE MAALUM LA KATIBA KUHUSIANA NA SURA YA KWANZA NA SURA YA SITA ZA RASIMU YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Filled under:

MAONI YA WAJUMBE WALIO WACHACHE WA KAMATI NAMBA SITA YA BUNGE MAALUM LA KATIBA KUHUSIANA NA SURA YA KWANZA NA SURA YA SITA ZA RASIMU YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA (Kwa mujibu wa Kanuni 32 (4) ya Kanuni za Bunge Maalum za Mwaka 2014) UTANGULIZI Sura ya Kwanza na Sura ya Sita za Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndizo msingi ambao Rasimu yote imejengwa juu yao. Hii ni kwa sababu Sura hizi mbili zinazungumzia mfumo na muundo wa Muungano. Katika Sura ya Kwanza, mfumo na muundo wa Muungano unatajwa kwenye...

Posted By Unknown07:21